Hamia kwenye habari

AGOSTI 7, 2018
MAREKANI

Moto wa Msituni Carr Waendelea Kuteketeza Eneo Karibu na Redding, California

Moto wa Msituni Carr Waendelea Kuteketeza Eneo Karibu na Redding, California

Moto mkubwa wa msituni unaendelea kuteketeza mali karibu na Redding, California, tangu ulipoanza kuwaka Julai 23, 2018. Moto huo, uliopewa jina la eneo ulioanzia, umeua watu wanane, na kuteketeza eneo lenye ukubwa wa ekari 110,000, na kuharibu majengo zaidi ya 1,300.

Wahubiri wanaoishi katika eneo lililoathiriwa hawajapata majeraha makubwa, ingawa ndugu mmoja alipata majeraha alipoendesha mashine ya kuchimba ili kuwasaidia wanaojaribu kuzima moto huo. Pia, ndugu na dada 454 wamepoteza makao na wanaishi kwenye nyumba za watu wa ukoo au wahubiri wengine. Nyumba za familia 12 za Mashahidi zimeteketea kabisa.

Wahubiri wote wako salama, na waangalizi wa mzunguko pamoja na wazee wa makutaniko wanashirikiana kuwaandalia ndugu zetu msaada wa kiroho unaohitajiwa na wa kimwili katika kipindi hiki chenye mkazo.—Methali 17:17.