Hamia kwenye habari

SEPTEMBA 20, 2018
MAREKANI

Dhoruba Florence Yapiga Eneo la Kusini-mashariki mwa Marekani

Dhoruba Florence Yapiga Eneo la Kusini-mashariki mwa Marekani

Dhoruba Florence imesababisha mafuriko katika sehemu kubwa za North Carolina, South Carolina, na majimbo mengine. Dhoruba hiyo ilikuwa kubwa sana, iliua watu 32 hivi na maelfu ya watu walipoteza makao.

Ofisi ya tawi ya Marekani inaripoti kwamba hakuna mhubiri yeyote aliyeuawa au kujeruhiwa na dhoruba hiyo, ingawa Mashahidi zaidi ya 4,000 wamepoteza makao. Hali zinaendelea kuwa bora, ingawa bado sehemu fulani haziwezi kufikiwa kwa sababu ya mafuriko. Uchunguzi unaonyesha kwamba dhoruba hiyo imeharibu nyumba 351 za ndugu zetu na Majumba ya Ufalme 21.

Halmashauri ya Kutoa Msaada (DRC) inashughulikia mahitaji ya chakula, maji, mavazi, makao, na matibabu. Jitihada za kutoa msaada zinatia ndani vikosi viwili vya wafanyakazi wa kuondoa miti. Kwa sababu ya mafuriko, wajitoleaji kutoka makutaniko ya eneo hilo na wengine walioalikwa wanafika ili kusaidia na watafanya kazi chini ya mwongozo wa DRC. Wazee na waangalizi wa mzunguko wanafanya ziara za uchungaji kwa wale walioathiriwa.

Tunasali kwa ajili ya ndugu na dada zetu wanaokabiliana na hali hiyo ngumu kwa sababu ya dhoruba hiyo na tunatazamia kwa hamu wakati ambapo ‘hatutaogopa.’—Isaya 12:2.