Hamia kwenye habari

FEBRUARI 26, 2018
MAREKANI

Habari za Karibuni Kuhusu Jitihada za Kutoa Msaada Baada ya Kimbunga Harvey

Habari za Karibuni Kuhusu Jitihada za Kutoa Msaada Baada ya Kimbunga Harvey

NEW YORK—Wakaaji wa Texas, Marekani wanaendelea kukabiliana na hali baada ya Kimbunga Harvey, kilichopiga eneo la Corpus Christi Agosti 25, 2017. Halmashauri mbili za Kutoa Msaada zinaongoza kazi ya kuwasaidia maelfu ya ndugu na dada walioathiriwa.

Ndugu akitafuta Mashahidi wa Yehova katika kituo cha kutoa msaada cha Houston, Texas.

Zaidi ya wajitoleaji 7,000 walisaidia katika jitihada za awali za usafi ambazo zilifanywa katika nyumba 2,300 za wahubiri. Kila juma, wajitoleaji 1,000 hivi wanasaidia katika kazi kubwa zaidi ya kurekebisha majengo yaliyoharibiwa. Kufikia sasa, wamerekebisha Majumba 48 ya Ufalme, na zaidi ya nyumba 545 zitafanyiwa marekebisho katika miezi ijayo. Inakadiriwa kwamba kazi ya kutoa msaada itagharimu dola milioni 8.5 katika eneo hilo tu na kazi hiyo itakamilika kufikia Juni 30, 2018.

Tangu mwishoni mwa Agosti 2017, jumla ya wawakilishi 22 wa ofisi ya tawi, kutia ndani washiriki 7 wa Halmashauri ya Tawi, wametembelea maeneo yaliyoathiriwa kuwaona wahubiri walioathiriwa ili kuwaimarisha na kuwafariji kupitia Biblia. Tunasali kwamba wote wanaohusika katika jitihada za kutoa msaada watatiwa nguvu ili kufanya kazi.—Nehemia 6:9.

Wafanyakazi wa kutoa msaada katika eneo la Aransas Pass, Texas.

Wanahabari Wanaweza Kuwasiliana na:

David A. Semonian, Ofisi ya Habari za Umma, +1-845-524-3000