Hamia kwenye habari

NOVEMBA 6, 2017
MAREKANI

Habari za Karibuni Kuhusu Moto wa California

Habari za Karibuni Kuhusu Moto wa California

Moto wa msituni katika eneo la California umedhibitiwa sasa, na Halmashauri ya Tawi ya Marekani imeandaa habari za karibuni kuhusu ndugu zetu katika eneo hilo.

Hakuna ndugu au dada aliyekufa, lakini ndugu wanane waliumia na wengine 1,400 walipoteza makao. Pia, nyumba 29 za ndugu zetu ziliharibiwa kabisa. Ndugu wote waliopoteza makao walitunzwa na Mashahidi katika makutaniko na mizunguko jirani, na wengi wao wamerudi nyumbani kwao.

Moto ulipokuwa unawaka bado, wawakilishi kutoka ofisi ya tawi waliwatembelea waangalizi wa mizunguko, Hamashauri za Kutoa Msaada, na wajitoleaji wenyeji wa kutoa msaada. Watu wa familia waliopoteza nyumba zao walitembelewa na kutiwa moyo. Isitoshe, mikutano ya pekee ilipangwa ili kuwafariji kupitia Maandiko na kuwategemeza wengi walioombwa kuwategemeza waliohamishwa.

Tuna uhakika kwamba Yehova ataendelea kuwafariji na kuwategemeza ndugu zetu wanapokabiliana na hali hii ngumu.—2 Wakorintho 1:3, 4.

David A. Semonian, Ofisi ya Habari za Umma, simu +1-845-524-3000