Hamia kwenye habari

MEI 22, 2017
MAREKANI

Siku ya Wageni Katika Makao Makuu Mapya ya Mashahidi Ilifurahiwa na Jamii

Siku ya Wageni Katika Makao Makuu Mapya ya Mashahidi Ilifurahiwa na Jamii

NEW YORK—Jumamosi, Aprili 29, 2017, Mashahidi wa Yehova walikuwa na siku ya pili ya wageni katika makao makuu mapya Warwick, New York, na ilihudhuriwa na watu wengi kuliko siku ya kwanza.

Kulikuwa na wageni 468 waliohudhuria tukio hilo Jumamosi iliyopita, ongezeko la asilimia 18 juu ya wale waliofika Jumamosi ya kwanza. “Tulifurahi sana kwamba majirani wengi, hasa maofisa wa mji, walifika na kutembelea majengo yetu yaliyokamilika,” anasema Troy Snyder, msimamizi wa majengo ya makao makuu. “Tulikuwa pia na wakaaji wa eneo hilo waliorudi kutembelea eneo hilo wakitegemea mambo waliyoona katika siku ya kwanza ya wageni.”

Ingrid Magar

Siku hizo mbili za wageni, zilizofanywa Jumamosi mbili zilizofuatana kati ya saa 4:00 asubuhi na saa 10:00 mchana, zilikuwa na jumla ya wahudhuriaji 863. Bw. Snyder anasema hivi: “Siku za wageni zilikuwa na matokeo mazuri. Wengi waliohudhuria walieleza jinsi walivyofurahia. Tunatazamia kwa hamu kuwakaribisha majirani wetu wakati mwingine wakipenda kutembelea eneo letu na vitu vya kale kuhusiana na Biblia.”

Ingrid Magar, mkaaji wa eneo lililo karibu la Tuxedo Park, New York, ni mmoja kati ya majirani wengi waliokaribishwa. Alikuwa amefanyia kazi kampuni inayoitwa Nickel iliyomiliki eneo hilo mapema. Alifanya kazi ya utafiti kwa miaka 18 katika maabara yao ya kuchunguza chuma. Akikumbuka jinsi ambavyo eneo hilo lilitumiwa, anasema hivi: “Nimefurahia ujenzi wa eneo la Warwick. Lilikaa muda mrefu bila kutumiwa na haikujulikana lingetumiwaje. Ni eneo maridadi na mmeliboresha.” Bi. Magar pia alisema hivi kuhusu wakaaji wapya: “Ninahisi kwamba ninyi [Mashahidi wa Yehova] ni majirani wazuri. Mna fadhili, mnajali mazingira, mnawajali majirani, na nahisi kwamba ni pendeleo kubwa kuwa na majirani kama ninyi.”

William Hoppe

“Ilikuwa wazi kwamba walitaka kufanya kazi yenye ubora wa hali ya juu kabisa.  . . . Hilo linaonekana wazi katika majengo yaliyokamilika,” akasema William Hoppe, mhandisi aliyekagua mradi wa Mji wa Warwick katika miaka miwili ya mwisho ya ujenzi. “Nimeshangazwa sana na jinsi walivyotunza mazingira wakati wa ujenzi, na kudumisha, na jinsi walivyo makini kuhusiana na mazingira katika ujenzi wote. Na ninafikiri ni mfano mzuri wa kuigwa na miradi mingine ya ujenzi itakayofanywa.”

Wanahabari Wanaweza Kuwasiliana na:

David A. Semonian, Ofisi ya Habari za Umma, +1-845-524-3000