Hamia kwenye habari

NOVEMBA 3, 2021
MEXICO

Kimbunga Pamela Chasababisha Mafuriko Katika Pwani ya Pasifiki ya Mexico

Kimbunga Pamela Chasababisha Mafuriko Katika Pwani ya Pasifiki ya Mexico

Oktoba 13, 2021, Kimbunga Pamela kilipiga eneo la pwani ya Mexico. Kimbunga hicho kilitokeza upepo mkali, mvua kubwa, na mafuriko hasa katika maeneo ya Durango, Nayarit, na Sinaloa.

Athari kwa Ndugu na Dada Zetu

  • Hakuna yeyote kati ya ndugu zetu aliyejeruhiwa

  • Wahubiri 112 walilazimika kuhama nyumba zao

  • Nyumba 75 zilipata uharibifu mdogo

  • Jumba 1 la Ufalme lilipata uharibifu mdogo

Jitihada za Kutoa Msaada

  • Ndugu zetu wanasema kwamba walikuwa wamejiandaa vizuri kwa ajili ya kimbunga hicho kwa sababu ya vikumbusho vinavyotolewa na tengenezo letu kuhusiana na misiba ya asili

  • Waliolazimika kuhama nyumba zao wamepata mahali pa kulala katika nyumba za watu wa ukoo au Mashahidi wenzao

  • Wahubiri 20 walipewa msaada wa chakula

  • Wazee wa eneo hilo wanawafanyia ziara za uchungaji wale walioathiriwa

  • Jitihada zote za kutoa msaada zinafanywa kupatana na miongozo ya usalama ya COVID-19

Upendo wa Yehova kuwaelekea ndugu zetu unaonekana wazi kutokana na jitihada za kutoa msaada zilizotolewa upesi sana. Kwa kweli Mungu wetu ni ‘kimbilio salama.’—Zaburi 59:16.