Hamia kwenye habari

JULAI 3, 2014
MEXICO

Mashahidi Washiriki Katika Maonyesho ya Vitabu na Magazeti ya Mexico City ya 2014

Mashahidi Washiriki Katika Maonyesho ya Vitabu na Magazeti ya Mexico City ya 2014

MEXICO CITY—Mashahidi wa Yehova walishiriki katika maonyesho yanayoitwa Expo Publica Book Fair, ambayo ndiyo ya kwanza kuandaliwa na Baraza la Kitaifa la Makampuni ya Uchapishaji ya Mexico (CANIEM). Maonyesho hayo yaliyofanyika katika majengo ya World Trade Center huko Mexico City kuanzia Aprili 25 hadi Mei 4, 2014, yaliadhimisha miaka 50 ya CANIEM. Watu 20,000 hivi walihudhuria maonyesho hayo.

Mashahidi walionyesha machapisho yao mbalimbali yanayotegemea Biblia—vitabu, magazeti, na video. Walionyesha pia Tovuti yao rasmi, www.pr418.com, ambamo machapisho yao yanaweza kupakuliwa katika lugha zaidi ya 650. Wageni walijichukulia zaidi ya machapisho 1,600 kutoka kwa Mashahidi, na baadhi yao wakaomba kutembelewa nyumbani kwao. Kama ilivyo kawaida ya Mashahidi wa Yehova, machapisho yao yote na funzo la Biblia la nyumbani yalitolewa bila malipo kwa waliohudhuria.

Gamaliel Camarillo, msemaji wa Mashahidi wa Yehova nchini Mexico, anasema: “Tulifurahi kwamba watu wengi sana walikuja kwenye meza yetu ya machapisho katika maonyesho hayo, na kusema wanapendezwa na Biblia na Tovuti yetu, jw.org. Tunahisi kwamba tunatumikia umma tunapowapatia watu wenye shughuli nyingi vifaa hivi muhimu wanapovitaka bila malipo. Tumepata matokeo makubwa kwa kushiriki maonyesho haya.”

Wanahabari Wanaweza Kuwasiliana na:

J. R. Brown, Ofisi ya Habari za Umma, simu +1 718 560 5000

Mexico: Gamaliel Camarillo, simu +52 555 133 3048