Hamia kwenye habari

NOVEMBA 28, 2014
MEXICO

Wenye Mamlaka Nchini Mexico Wawasifu Mashahidi kwa Kufanya Usafi Kwenye Uwanja wa Michezo

Wenye Mamlaka Nchini Mexico Wawasifu Mashahidi kwa Kufanya Usafi Kwenye Uwanja wa Michezo

MEXICO CITY—Zaidi ya Mashahidi wa Yehova 250 walijitolea kufanya usafi kwenye uwanja wa michezo wa Baldomero “Melo” Almada mwezi wa Juni 7, 2014, ili kuutayarisha kwa ajili ya tukio la kijamii la pekee. Wenye mamlaka waliwashukuru sana kwa kazi hiyo.

Kwa miezi mingi, Profesa Antonio Cota Márquez, mkurugenzi wa Taasisi ya Michezo ya Manispaa ya Huatabampo, Mexico, alitafuta wajitoleaji wa kusaidia kufanya usafi kwenye uwanja huo wa michezo kabla ya gavana kufungua rasmi njia mpya za wakimbiaji mwezi wa Julai 7, 2014. Mashahidi wa Yehova walimsaidia mkurugenzi huyo pamoja na wafanyakazi wa uwanja huo kufanya marekebisho mengi, kutia ndani kuondoa takataka, kupaka rangi upya ubao wa mpira wa kikapu, na kushughulikia bustani.

Ukumbi, ulio ndani ya uwanja wa michezo, mahali ambapo Mashahidi walifanyia programu za kujifunza Biblia bila malipo.

Mkurugenzi huyo anayeitwa Cota aliamua kuwasiliana na Mashahidi kwa sababu alijua jinsi wanavyotunza ukumbi mmoja katika uwanja huo wa michezo ambako wao hufanyia programu za elimu ya Biblia kwa ukawaida bila malipo katika Kihispania na Kimayo. Baada ya kuona jinsi Mashahidi walivyosafisha na kurekebisha uwanja huo, Mkurugenzi Cota alisema hivi alipohojiwa: “Tunafurahi kuona watu wasio na ubinafsi wakitumia wakati wao kusafisha uwanja wetu wa michezo.” Baadaye alisema hivi: “Kwa niaba ya meya, Ramón Díaz Nieblas, tafadhali pokeeni shukrani zetu kwa sababu ya kazi yenu leo. Tutaendelea kuwategemeza mnapotumia uwanja huu. Tunafurahishwa sana na kuwajibika kwenu na ushirikiano.”

Wanahabari Wanaweza Kuwasiliana na:

J. R. Brown, Ofisi ya Habari za Umma, simu +1 718 560 5000

Mexico: Gamaliel Camarillo, simu + 52 555 133 3000