Hamia kwenye habari

OKTOBA 6, 2022
MSUMBIJI

Tafsiri ya Ulimwengu Mpya Yatolewa Katika Lugha ya Sena

Tafsiri ya Ulimwengu Mpya Yatolewa Katika Lugha ya Sena

Oktoba 2, 2022, Ndugu David Amorim, mshiriki wa Halmashauri ya Tawi ya Msumbiji, alitoa Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya katika lugha ya Sena. a Biblia hiyo ilitolewa katika programu iliyorekodiwa mapema, na wahubiri wengi waliitazama katika Majumba yao ya Ufalme. Programu hiyo pia ilipeperushwa kwenye kituo cha televisheni cha kitaifa na kwenye vituo 14 vya redio.

Nchini Msumbiji, lugha ya Sena huzungumzwa katika mikoa minne: Manica, Sofala, Tete, na Zambezia. Lugha ya Sena huzungumzwa pia katika maeneo fulani ya Malawi.

Ofisi ya utafsiri ya lugha ya Sena iliyo Beira, Msumbiji

Hii ni mara ya kwanza kwa Mashahidi wa Yehova kutafsiri Biblia nzima ya Tafsiri ya Ulimwengu Mpya katika mojawapo ya lugha za asili za Msumbiji. Kabla ya Tafsiri ya Ulimwengu Mpya kutolewa, kulikuwa na tafsiri nyingine za sehemu fulani za Biblia katika lugha ya Sena, lakini zilikuwa ghali na zilitumia maneno ya kale.

Tunashangilia pamoja na ndugu na dada zetu wanaozungumza lugha ya Sena kwa sababu ya baraka hii ya pekee ambayo wamepata kutoka kwa Yehova.​—Methali 10:22.

a Biblia hiyo ilitolewa katika mfumo wa kielektroni na nakala zilizochapishwa zinapatikana pia.