Hamia kwenye habari

SEPTEMBA 12, 2016
NAGORNO-KARABAKH

Artur Avanesyan Amepata Msamaha na Kuachiliwa Kutoka Gerezani

Artur Avanesyan Amepata Msamaha na Kuachiliwa Kutoka Gerezani

Septemba 6, 2016, wenye mamlaka nchini Nagorno-Karabakh walimwachilia huru Artur Avanesyan mwenye umri wa miaka 20 kutoka katika gereza la Shushi, kwa kuwa alipata msamaha wa serikali. Bw. Avanesyan alikuwa ametumikia kifungo cha miezi 26 kati ya miezi 30 aliyohukumiwa kwa sababu ya kukataa kujiunga na jeshi. Ukweli ni kwamba alikuwa ameomba kufanya utumishi wa badala wa kiraia lakini wenye mamlaka walikataa kumpa nafasi hiyo. Kijana huyo alifurahi sana kuungana tena na familia yake.

Mashahidi wa Yehova wanafurahi sana kwamba Bw. Avanesyan ameachiliwa kutoka gerezani. Wanatumaini kwamba wenye mamlaka watatambua haki ya kukataa kujiunga na jeshi kwa sababu ya dhamiri na kuwapatia vijana wa Nagorno-Karabakh nafasi ya kufanya utumishi wa badala wa kiraia ikiwa hawataki kujiunga na jeshi.