Hamia kwenye habari

APRILI 29, 2014
NIKARAGUA

Matetemeko ya Nchi Nchini Nikaragua

Matetemeko ya Nchi Nchini Nikaragua

Jumatatu, Aprili 14, 2014, tetemeko la nchi lenye kipimo cha 5.1 kwenye kipimo cha Ritcher lilikumba eneo la Managua lililoko upande wa kaskazini magharibi wa nchi ya Nikaragua. Tetemeko hilo lilikuwa kati ya matetemeko ya karibuni zaidi kukumba nchi hiyo katika muda wa siku nne zilizokuwa zimetangulia, tetemeko kubwa zaidi likiwa na ukubwa wa 6.6 katika kipimo cha Ritcher. Ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova ya Amerika ya Kati iliyoko nchini Mexico imethibitisha kwamba hakuna Shahidi aliyejeruhiwa. Nyumba 7 za Mashahidi ziliharibiwa kabisa na nyingine 21 zikaathiriwa vibaya sana. Mjini Nagarote, Jumba moja la Ufalme (mahali pa ibada pa Mashahidi wa Yehova) liliharibiwa vibaya sana. Kwa sababu hiyo, makutaniko mawili ya Mashahidi wa Yehova yalilazimika kukutana kwenye eneo la kuegeshea magari la Jumba hilo la Ufalme kwa ajili ya mwadhimisho wa kila mwaka wa kifo cha Yesu Kristo. Jioni hiyo, zaidi ya watu 530 walihudhuria mwadhimisho huo, kutia ndani watu wengi ambao si Mashahidi wa Yehova. Ofisi ya tawi inaendelea kutoa msaada na makao ya muda kwa Mashahidi ambao nyumba zao ziliharibiwa.

Wanahabari Wanaweza Kuwasiliana na:

J. R. Brown, Ofisi ya Habari za Umma, simu +1 718 560 5000

Amerika ya Kati: Gamaliel Camarillo, simu +52 555 133 3048