Hamia kwenye habari

Mtaa uliojaa maji yaliyotokana na mafuriko hayo jijini Piura. Picha ndogo iliyo kushoto: Wajitoleaji wakirekebisha nyumba ya ndugu iliyo Cieneguilla. Picha ndogo iliyo kulia: Familia moja iliyoathiriwa na kimbunga hicho ikifurahia kitia-moyo kutoka kwa mshiriki wa Halmashauri ya Tawi aliyewatembelea

APRILI 12, 2023
PERU

Kimbunga Yaku Kimepiga Pwani ya Peru

Kimbunga Yaku Kimepiga Pwani ya Peru

Kimbunga Yaku kimepiga pwani ya kaskazini mwa Peru mwanzoni mwa mwezi wa Machi 2023. Kulikuwa na mafuriko na maporomoko ya ardhi kwa siku mbili, kisha hali ya hatari ikatangazwa katika mikoa iliyo kaskazini na iliyo kati nchini. Mafuriko hayo yameharibu nyumba, madaraja, na barabara kuu, na hivyo kufanya iwe vigumu hata zaidi kukimbia.

Athari Ambazo Ndugu na Dada Zetu Wamepata

  • Hakuna ndugu au dada aliyekufa

  • Wahubiri 2 wamejeruhiwa

  • Wahubiri 106 wamepoteza makao yao

  • Nyumba 70 ziliharibiwa

  • Nyumba 130 zilipata uharibifu mdogo

  • Majumba 5 ya Ufalme yameharibiwa

  • Majumba 5 ya Ufalme yalipata uharibifu mdogo

Jitihada za Kutoa Msaada

  • Waangalizi wa mzunguko wanashirikiana na wazee wa makutaniko katika maeneo hayo ili kuandaa msaada wa kiroho na wa kimwili kwa ajili ya wale walioathiriwa

  • Halmashauri 3 za Kutoa Msaada zilianzishwa ili kuratibu kazi hiyo

Tuna uhakika kwamba Yehova anawasaidia ndugu zetu nchini Peru “[kuvumilia] kikamili kwa subira na shangwe.”​—Wakolosai 1:11.