Hamia kwenye habari

Wawakilishi wawili wa Ubalozi wa Thailand (katikati kulia) walipigwa picha pamoja na washiriki wa ofisi ya tawi na Mashahidi wanaoishi katika karibu walipotembelea ofisi ya tawi

OKTOBA 9, 2018
PERU

Ubalozi wa Thailand Watoa “Shukrani Nyingi na Pongezi” kwa Mashahidi wa Yehova Nchini Peru kwa Kuwasaidia Raia wa Thailand Waliofungwa

Ubalozi wa Thailand Watoa “Shukrani Nyingi na Pongezi” kwa Mashahidi wa Yehova Nchini Peru kwa Kuwasaidia Raia wa Thailand Waliofungwa

Juni 26, 2018, wawakilishi wa Ubalozi wa Thailand nchini Peru walitembelea ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova iliyoko kwenye mji mkuu, Lima. Kusudi lao lilikuwa kuwashukuru akina ndugu kwa kuwasaidia raia wa Thailand walio katika magereza ya Peru.

Tangu 2007, Mashahidi wa Yehova nchini Peru wamekuwa wakitembelea magereza wanapofanya kazi ya kutoa elimu ya Biblia. Lakini kuanzia 2013, akina ndugu wamekuwa wakitembelea gereza ambalo lina wafungwa kutoka Thailand. Kwa sababu ya kuvutiwa na upendezi huo wa kibinafsi, maofisa wa ubalozi wa Thailand waliwasiliana na ofisi ya tawi na kupanga kutembelea ofisi yetu.

Ndugu na dada wakiondoka gerezani ambako walisaidia wafungwa kujifunza mengi zaidi kuhusu Biblia.

Msafara kutoka kwenye ubalozi ulitia ndani Bw. Angkura Kulvanij, naibu wa balozi; Bw. Pathompong Singthong, katibu wa kwanza; na Bi. Pradthana Pongudom, msaidizi wa kibalozi. Washiriki wa Halmashauri ya Tawi waliandamana nao walipokuwa wakitembea, na wakaelezwa jinsi ofisi ya tawi inavyoshughulikia kazi kubwa ya kutafsiri, inayotia ndani kutafsiri machapisho yetu katika lugha tisa nchini humo.

Wawakilishi wa Ubalozi wa Thailand watazama huku ndugu akitafsiri machapisho yetu katika Lugha ya Ishara ya Peru.

Katika barua rasmi kwa ofisi ya tawi, ubalozi ulitoa “shukrani nyingi na pongezi” kwa bidii ya akina ndugu ya kuwatunza “wasiojiweza na wanaoweza kuathiriwa kwa urahisi nchini Peru, bila kujali imani au utamaduni wao.” Pia ubalozi ulipongeza “jitihada nyingi na michango ya wafanyakazi wa Association of Jehovah’s Witnesses, katika ofisi ya tawi ya Peru, ili kusaidia kupunguza hali ngumu na kuboresha maisha ya wafungwa ambao ni raia wa Thailand.”

Jambo hilo ambalo ndugu zetu walijionea nchini Peru linaonyesha matokeo mazuri ya kuendelea kuwahubiria watu wa namna zote ujumbe wa Biblia.—1 Wakorintho 9:22.