Hamia kwenye habari

Mlima wa volkano ulio chini ya maji ulilipuka karibu na nchi ya Tonga, ukafunika visiwa hivyo kwa majivu. Tsunami iliyotokea ilisababisha uharibifu mkubwa

JANUARI 26, 2022
TONGA

Mlipuko wa Mlima wa Volkano na Tsunami Zasababisha Madhara Nchini Tonga

Mlipuko wa Mlima wa Volkano na Tsunami Zasababisha Madhara Nchini Tonga

Januari 15, 2022, tsunami kubwa ilipiga kisiwa cha Tonga baada ya mlima wa volkano ulio chini ya maji kulipuka kwenye Bahari ya Pasifiki. Athari zake zilisikika hadi Amerika Kusini na Japani. Majivu na mafuriko yamesababisha madhara katika eneo kubwa la Tonga, na mawasiliano yamekatizwa.

Athari Ambazo Ndugu na Dada Zetu Wamepata

  • Hakuna ndugu au dada aliyejeruhiwa

Jitihada za Kutoa Msaada

  • Halmashauri ya Kutoa Msaada ilianzishwa

  • Akina ndugu wanawasaidia wale walioathiriwa kuondoa majivu kwenye paa zao kwa kuwa michirizi huwasaidia kukinga maji ya kunywa

  • Jitihada zote za kutoa msaada zinafanywa kupatana na miongozo ya usalama ya COVID-19

Akina ndugu wamerudia ratiba ya kiroho upesi na wanaongoza mikutano kwa ukawaida. Tunajua kwamba Yehova atathibitika kuwa “msaidizi . . . na mfariji” kwa ndugu na dada zetu walioathiriwa na janga hilo.​—Zaburi 86:17.