Hamia kwenye habari

OKTOBA 29, 2018
UFARANSA

Mafuriko ya Ghafla Ufaransa Kusini

Mafuriko ya Ghafla Ufaransa Kusini

Oktoba 14 na 15, 2018, mvua kubwa ilinyesha katika eneo la kusini mwa Ufaransa na hivyo kusababisha mafuriko makubwa ambayo yamesababisha vifo vya watu 10 hivi.

Ofisi ya tawi ya Ufaransa inaripoti kwamba ndugu wote wanaoishi katika eneo hilo wako salama, ingawa familia fulani zilihamishwa wakati wa mafuriko hayo. Baadhi ya Mashahidi wamesema kwamba mali zao ziliharibika kidogo; majengo matatu yaliharibika kwa kiwango kikubwa. Dawati la Kutoa Msaada Wakati wa Misiba kwenye ofisi ya tawi limekuwa likiwategemeza akina ndugu.

Tunaendelea kuwa na uhakika kwamba mkono wenye nguvu wa Mungu wetu, Yehova, ‘utawashika kwa nguvu’ ndugu zetu wanaoendelea kushikamana naye wakati huu wenye mkazo.—Zaburi 63:8.