Hamia kwenye habari

NOVEMBA 4, 2014
UGIRIKI

Habari Kuhusu Kusanyiko la Kimataifa: Mashahidi wa Yehova Wakusanyika Katika Uwanja wa Olympic Nchini Ugiriki

Habari Kuhusu Kusanyiko la Kimataifa: Mashahidi wa Yehova Wakusanyika Katika Uwanja wa Olympic Nchini Ugiriki

Samuel Herd (kulia), mshiriki wa Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova alitoa hotuba za mwisho kila siku na zikatafsiriwa katika Kigiriki.

Kulikuwa pia na ubatizo siku ya Jumamosi, Juni 28; jumla ya watu 337 walibatizwa, 305 walibatizwa nchini Ugiriki na watu 32 walibatizwa nchini Saiprasi.

ATHENS, Ugiriki—Mashahidi wa Yehova nchini Ugiriki walifanya Kusanyiko la Kimataifa lenye kichwa “Endeleeni Kuutafuta Kwanza Ufalme wa Mungu!” katika Uwanja wa Olympic Athletic Center huko Athens. Huo ndio uwanja uliotumiwa pia kwa ajili ya Michezo ya Olimpiki ya mwaka wa 2004 iliyofanyika Juni 27-29, 2014. Watu 35,863 walikusanyika katika uwanja huo. Wakati wa sehemu fulani za programu hiyo, watu wengine 3,093 waliunganishwa kupitia video nchini Saiprasi na Ubelgiji, kwa hiyo jumla ya wahudhuriaji ilikuwa 38,956.

Wajumbe kutoka Afrika Kusini, Hungaria, Korea, Kroatia, Marekani, Rumania, na Uturuki walihudhuria kusanyiko hilo. Christina Michail, msimamizi wa sehemu kuu ya uwanja wa Olympic, alisema hivi: “Lilikuwa jambo lenye kupendeza sana kuwaona watu wa rangi tofauti na kutoka nchi tofauti, wakiwa wameketi pamoja na wakipiga picha pamoja; nilifurahia sana kuona upendo uliokuwepo kati yao . . . Hilo ni jambo la pekee sana. Si kawaida kuona hivyo katika uwanja huu. Kwa kawaida mashabiki wa michezo ndio huja katika uwanja huu, na tabia yao ni tofauti kabisa; tulifurahia kuona watu tofauti.”

Wahudhuriaji wa kusanyiko katika Olympic Athletic Center jijini Athens.

Robert Kern, msemaji wa ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova nchini Ugiriki, alisema hivi: “Tumepokea barua nyingi za shukrani kwa ajili ya programu ya kusanyiko hilo na pia nafasi ya kufurahia ushirika pamoja na ndugu zetu wa mataifa mbalimbali. Ilifurahisha sana kuwa pamoja na waabudu wenzetu kutoka nchi nyingine kwa ajili ya tukio hili la pekee sana.”

Wanahabari Wanaweza Kuwasiliana na:

J. R. Brown, Ofisi ya Habari za Umma, simu +1 718 560 5000

Ugiriki: Babis Andreopoulos, simu +30 210 617 8606