Hamia kwenye habari

Dada Helen Budge akitumia kifaa cha kuandikia maandishi ya vipofu

MACHI 24, 2021
UINGEREZA

Kushiriki Kampeni ya Ukumbusho Licha ya Ulemavu

Kushiriki Kampeni ya Ukumbusho Licha ya Ulemavu

Helen Budge, Shahidi wa Yehova kutoka Edinburgh, Scotland, ni kipofu. Kama ilivyo kwa Mashahidi wote wa Yehova, vizuizi vinavyotokana na ugonjwa wa virusi vya corona vinamzuia Helen kushiriki katika huduma kwa kuwatembelea watu uso kwa uso. Lakini hilo halijamzuia kufanya yote awezayo katika kampeni ya kuwaalika watu kwenye Ukumbusho wa kifo cha Yesu.

Ili kushiriki, Helen huandika habari ambazo angependa zitiwe katika barua zake akitumia kifaa cha kuandika maandishi ya vipofu. Anaeleza hivi, “Kwa maoni yangu kufanya hivyo ni sawa na kutumia penseli na karatasi.” Kisha Helen hutumia habari hizo kumwambia mpwa wake mambo atakayomwandikia kwenye barua.

Mwaliko wa Ukumbusho katika maandishi ya vipofu

Kwa kuwa mama na nyanya ya Helen ni Mashahidi wa Yehova, sikuzote Ukumbusho umekuwa sehemu muhimu ya maisha yake. Helen anaeleza kwamba yeye hutazamia kwa hamu kuwaalika wengine kwenye tukio hilo. Anasema hivi: “Mwaka huu nitahudhuria Ukumbusho kwa mara ya 70. Kila mwaka mimi hufurahi sana kupokea nakala ya mwaliko wa Ukumbusho katika maandishi ya vipofu. Ninasoma mwaliko huo ili kuelewa habari zilizomo. Kisha ninaanza kufikiria nitamwalika nani.”

Hata hali iweje, Wakristo waaminifu ulimwenguni pote wanachochewa na upendo kuwaalika majirani wao kuhudhuria Ukumbusho wa kifo cha Kristo Jumamosi, Machi 27.—Luka 22:19.