Hamia kwenye habari

UKRAINIA

Maelezo Mafupi Kuhusu Ukrainia

Maelezo Mafupi Kuhusu Ukrainia

Mashahidi wa Yehova wamekuwepo nchini Ukrainia kwa zaidi ya karne moja. Walisajiliwa rasmi kisheria Februari 28, 1991, muda mfupi baada ya Ukrainia kupata uhuru.

Utawala wa Nazi na Sovieti uliwapinga sana Mashahidi wa Yehova nchini Ukrainia. Aprili 8, 1951, serikali ya Sovieti iliwahamisha Mashahidi zaidi ya 6,100 kutoka eneo la magharibi mwa Ukrainia mpaka Siberia. Hali ilianza kutulia Juni 1965 baada ya Mahakama kuu ya Ukrainia kutangaza kwamba machapisho ya Mashahidi wa Yehova yanazungumzia habari za dini wala si za kupinga serikali ya Sovieti. Serikali iliacha kuwafunga watu kwa sababu ya kusoma machapisho ya Mashahidi lakini iliendelea kuwafunga Mashahidi wa Yehova kwa sababu ya kuzungumza na watu wengine kuhusu imani yao. Septemba 1965, Mashahidi wote ambao walipelekwa uhamishoni mwaka 1951 huko Siberia walipata msamaha wa serikali, lakini wengi wao hawakuruhusiwa kurudi nyumbani kwao. Mapema miaka ya 1980 Mashahidi walianza kuteswa tena.

Leo, Mashahidi wa Yehova wanafurahia uhuru wa kukusanyika pamoja kwa ajili ya ibada na kuhubiri hadharani bila kupingwa na mamlaka. Hata hivyo, Mashahidi wanatendewa vibaya kwa sababu ya chuki. Serikali haijachukua hatua yoyote ili kuwalinda Mashahidi kutokana na mashambulizi wanayofanyiwa kibinafsi na katika nyumba zao za ibada, na katika visa vingi serikali haiwashtaki wakosaji. Kwa sababu ya kutochukuliwa hatua yoyote wahalifu hao wanafanya jeuri kwa uhuru kabisa. Pia, kwa kuwa eneo la mashariki mwa nchi hiyo lina migogoro, hali hiyo imesababisha mashambulizi dhidi ya Mashahidi yaongezeke.