Hamia kwenye habari

NOVEMBA 11, 2014
UKRAINIA

Licha ya Vita Mashahidi wa Yehova Nchini Ukrainia Wakusanyika kwa Amani; Biblia Yatolewa

Licha ya Vita Mashahidi wa Yehova Nchini Ukrainia Wakusanyika kwa Amani; Biblia Yatolewa

Anthony Morris, mshiriki wa Baraza Linaloongoza akitangaza kutolewa kwa Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya iliyorekebishwa.

LVIV, Ukrainia—Licha ya vita vinavyoendelea Ukrainia mashariki, Mashahidi wa Yehova walikusanyika jijini Lviv kuanzia Julai 4-6, 2014, kwa ajili ya Kusanyiko la Eneo lenye kichwa “Endeleeni Kuutafuta Kwanza Ufalme wa Mungu!” Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya iliyorekebishwa, katika Kiukrainia cha kisasa, ilitolewa na Anthony Morris, mshiriki wa Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova.

Ofisi ya tawi ya Mashahidi nchini humo ilipanga sehemu kuu za kusanyiko hilo ziunganishwe kupitia video katika majiji 8 na sehemu nyingine 62 zilizo katika eneo la Donetsk, ambako vita vimepamba moto. Kwenye uwanja wa Lviv, kilele cha watu 18,336 walihudhuria. Jumla ya watu waliohudhuria ilikuwa 82,832 kutia ndani maeneo yaliyounganishwa. Watu 1,068 walibatizwa.

Jumla ya watu 18,336 walihudhuria Kusanyiko la “Endeleeni Kuutafuta Kwanza Ufalme wa Mungu!” katika uwanja wa michezo jijini Lviv.

Siku ya kwanza ya kusanyiko, programu ilikatizwa kwa sababu ilisemekana kuna bomu lililotegwa katika uwanja huo, na hivyo watu wote wakaondoka uwanjani mara moja. Zaidi ya watu 16,000 waliondoka katika uwanja huo wa michezo katika muda wa dakika 11 tu, lakini programu iliendelea upesi tu baada ya wenye mamlaka kuhakikisha kwamba ulikuwa uvumi tu.

Vasyl Kobel, msemaji wa Mashahidi wa Yehova nchini Ukrainia, anasema: “Tulifurahi kuwa na wageni wengi sana katika kusanyiko letu. Jambo kuu la kusanyiko hilo lilikuwa kupokea Tafsiri ya Ulimwengu Mpya iliyorekebishwa katika Kiukrainia, ambayo ilitolewa kwa mara ya kwanza katika Kiingereza mwaka wa 2013. Tunafurahia sana kuwaeleza majirani wetu kuhusu ahadi ya Biblia kwamba kutakuwa na wakati ujao wenye amani, hasa kwa sababu ya hali ya msukosuko inayokabili nchi yetu kipindi hiki.”

Wanahabari Wanaweza Kuwasiliana na:

J. R. Brown, Ofisi ya Habari za Uma, simu +1 718 560 5000

Ukrainia: Vasyl Kobel, simu +38 032 240 9323