Hamia kwenye habari

JULAI 25, 2017
UKRAINIA

Maofisa Wahudhuria Siku ya Wageni ya Mashahidi wa Yehova Nchini Ukrainia

Maofisa Wahudhuria Siku ya Wageni ya Mashahidi wa Yehova Nchini Ukrainia

LVIV, Ukrainia—Ofisi ya tawi ya Ukrainia ya Mashahidi wa Yehova iliwakaribisha watu kwa ajili ya siku ya pekee ya wageni Mei 2, 2017. Tukio hilo la siku moja liliwaruhusu maofisa wa serikali na maofisa wengine, wasomi, wafanyabiashara, na majirani waone kazi inayofanywa katika ofisi hiyo jijini Lviv.

Siku ya wageni ilitia ndani maonyesho kwa ajili ya watoto.

Ofisi ilitayarisha maonyesho ya pekee kwa ajili ya siku hiyo, yaliyotia ndani mabango na video kuhusu utendaji wa ofisi hiyo, hifadhi ya vitu vya kale, na sehemu kwa ajili ya watoto. Ivan Riher, msemaji wa Mashahidi wa Yehova nchini Ukrainia, alisema hivi: “Hii ni mara ya kwanza tangu mwaka wa 2001 ambayo ofisi yetu ya tawi imekuwa na siku ya wageni. Tunajulikana sana nchini Ukrainia kwa kazi yetu ya kutoa elimu ya Biblia nyumba kwa nyumba, lakini tulitazamia kwa hamu kuwakaribisha majirani wetu waone kazi inayofanywa katika ofisi yetu ya tawi na jinsi kazi hiyo inavyochangia maendeleo ya jamii.”

Waliohudhuria walielezwa kuhusu historia ndefu ya Mashahidi wa Yehova nchini Ukrainia katika hifadhi ya vitu vya kale.

Andriy Yurash, msimamizi wa Idara ya Masuala ya Kidini na Kitaifa.

Andriy Yurash, msimamizi wa Idara ya Masuala ya Kidini na Kitaifa, ambayo ni idara katika Wizara ya Utamaduni wa Ukrainia, alieleza hivi maoni yake kuhusu utendaji wa ofisi ya tawi: “Hiki ni kielelezo kilichowekwa na shirika la Mashahidi wa Yehova, kikionyesha mambo yanayoweza kufanywa kupatanisha uhusiano katika jamii, na kati ya washiriki wake na watu wengine kwa ujumla.”

Mwaka huu, Mashahidi wamekuwa na siku za wageni katika ofisi zao za tawi nchini Kamerun, na vilevile katika makao makuu ulimwenguni pote huko Warwick, New York.

Wanahabari Wanaweza Kuwasiliana na:

David A. Semonian, Ofisi ya Habari za Umma, simu +1-845-524-3000

Ukrainia: Ivan Riher, simu +38-032-240-9323