Hamia kwenye habari

NOVEMBA 21, 2014
UKRAINIA

Taarifa: Mashahidi wa Yehova Watoa Msaada kwa Maelfu ya Watu Waliokosa Makao Huko Ukrainia

Taarifa: Mashahidi wa Yehova Watoa Msaada kwa Maelfu ya Watu Waliokosa Makao Huko Ukrainia

LVIV, Ukrainia—Mashahidi wa Yehova waendelea kuwasaidia waabudu wenzao waliokosa makao kwa sababu ya vita vinavyondelea katika eneo la mashariki mwa Ukrainia.

Karibu watu 7,500 wamehama eneo hilo, na 4,000 hivi kati yao wanatunzwa na halmashauri saba za kutoa msaada zilizopangwa na ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova ya Lviv. Wengine wanaishi na watu wa familia na Mashahidi wenzao huko Ukrainia na Urusi. Halmashauri nyingine sita za kutoa msaada zinawatunza zaidi ya Mashahidi 17,500 ambao bado wanaishi katika eneo hilo la vita.

Mabomu yaliyaharibu nyumba kadhaa za Mashahidi, kutia ndani nyumba hii katika kijiji cha Semenivka, katika eneo la Donetsk.

Ofisi ya tawi ya Lviv imesema kwamba jumla ya Mashahidi sita wamekufa tangu kuanza kwa vita hivyo. Shahidi mmoja katika eneo la Kramatorsk alikufa Juni 17, 2014, bomu lilipolipuka karibu na gari ambalo alikuwa ndani yake. Mabomu mengine yaliwaua Mashahidi watano walioishi katika majiji ya Donetsk, Sloviansk, Rozkishne, na Luhansk.

Kama njia ya kutoa msaada, ofisi ya tawi inaendelea kufanya mipango ya kujenga tena majengo kadhaa ya ibada na makao kwa ajili ya Mashahidi hao.

Mashahidi wakirekebisha paa la nyumba iliyoharibiwa katika jiji la Sloviansk.

Wanahabari Wanaweza Kuwasiliana na:

J. R. Brown, Ofisi ya Habari za Umma, simu +1 718 560 5000

Ukrainia: Vasyl Kobel, simu +38 032 240 9323