Hamia kwenye habari

JULAI 18, 2014
UKRAINIA

Ripoti Kuhusu Ukrainia na Crimea

Ripoti Kuhusu Ukrainia na Crimea

LVIV, Ukrainia—Ofisi ya Tawi ya Mashahidi wa Yehova nchini Ukrainia inaripoti kwamba Juni 17, 2014, Shahidi mmoja katika jiji la Ukrainia mashariki liitwalo Kramatorsk aliuawa na bomu lililolipuka karibu na gari lake. Hakuna Shahidi mwingine aliyeuawa au kujeruhiwa vibaya kutokana na vita vya wenyewe kwa wenyewe vinavyoendelea nchini humo vilivyoanza miezi michache iliyopita. Hata hivyo, mamia ya Mashahidi wamehamishwa kutoka katika maeneo yaliyoathiriwa ya mashariki mwa Ukrainia. Mashahidi walioathiriwa wanaishi na waabudu wenzao.

Licha ya mapigano yanayoendelea, Mashahidi nchini Ukrainia wanaendelea kuwahubiria jirani zao kuhusu ujumbe wa Biblia unaofariji. Mwanzoni mwa Juni 2014, Mashahidi walifanya makusanyiko mengi makubwa kwa amani mashariki mwa Ukrainia, yaliyotia ndani hotuba zinazotegemea Biblia na maonyesho ya jinsi ya kutumia mashauri ya Biblia kila siku maishani. Watu zaidi ya 5,200 walihudhuria. Mashahidi nchini Ukrainia na Crimea wamepanga kufanya makusanyiko 40 hivi ya eneo, yatakayokazia ahadi inayotolewa na Biblia kuhusu wakati ujao wenye amani chini ya Ufalme wa Mungu. Watu zaidi ya 165,000 wanatarajiwa kuhudhuria makusanyiko hayo, kutia ndani watu 7,500 katika Crimea.

Wanahabari Wanaweza Kuwasiliana na:

J. R. Brown, Ofisi ya Habari za Umma, simu +1 718 560 5000

Ukrainia: Vasyl Kobel, simu +38 032 240 9323