Hamia kwenye habari

Mkutano kwenye Jumba la Ufalme kabla ya janga la COVID-19

OKTOBA 15, 2021
HABARI ZA ULIMWENGUNI POTE

Baraza Linaloongoza Limetangaza Mikutano Fulani Inaweza Kuanza Tena Katika Maeneo Yaliyochaguliwa

Baraza Linaloongoza Limetangaza Mikutano Fulani Inaweza Kuanza Tena Katika Maeneo Yaliyochaguliwa

Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova limetangaza kwamba ofisi fulani za tawi zimeombwa kushiriki katika programu ya majaribio itakayoruhusu makutaniko fulani yaanze kukutana tena kwa ajili ya mikutano fulani ya kutaniko. Ofisi za tawi zinazoshiriki katika programu hiyo zitateua Majumba ya Ufalme katika maeneo ambako watu wengi sana wamepata chanjo na ambako kiwango cha maambukizi kiko chini. Bila shaka, kila sehemu ya programu hiyo itafanywa kupatana na miongozo ya serikali kwa ajili ya mikusanyiko katika eneo hilo. Tangazo hilo lilitolewa kwa familia zote za Betheli ulimwenguni, Ijumaa, Oktoba 15, 2021.

Matokeo ya programu hiyo ya majaribio yataonyesha ikiwa makutaniko ya ziada yataruhusiwa kuanza kukutana tena pamoja. Tangazo hilo lilisema pia kwamba kwa ujumla, bado utendaji wa kitengenezo unaofanywa uso kwa uso utaendelea kusitishwa hadi angalau Januari 1, 2022.

Tunathamini sana jinsi Baraza Linaloongoza linavyotunza undugu wetu wa ulimwenguni pote na jinsi wanavyotumia hekima kufanya majaribio kabla ya kurudia utendaji wa kitengenezo. Tafadhali endeleeni kutoa sala kwamba Yehova aongoze na kubariki mipango hiyo.—Methali 14:16.