Hamia kwenye habari

Kutoka kushoto kwenda kulia: Ndugu Vladimir Maladyka; Ndugu Vladimir Sakada na mke wake, Svetlana; Ndugu Yevgeniy Zhukov

MEI 9, 2022
HABARI ZA ULIMWENGUNI POTE

HABARI ZA KARIBUNI—NDUGU WANAFUNGWA | Familia Huko Crimea Zinaendelea Kuvumilia kwa Msaada wa Yehova

HABARI ZA KARIBUNI—NDUGU WANAFUNGWA | Familia Huko Crimea Zinaendelea Kuvumilia kwa Msaada wa Yehova

Oktoba 6, 2022, Mahakama ya Wilaya ya Nakhimovskiy iliyo Sevastopol iliwahukumu Ndugu Vladimir Maladyka, Ndugu Vladimir Sakada, na Ndugu Yevgeniy Zhukov. Kila mmoja wao alihukumiwa kifungo cha miaka sita gerezani. Hukumu yao ilianza mara moja.

Mfuatano wa Matukio

  1. Oktoba 1, 2020

    Maofisa wa FSB walivamia nyumba tisa za Mashahidi wa Yehova zilizo Sevastopol, kutia ndani nyumba ya familia ya Maladyka, ya Sakada, na ya Zhukov. Walipofanya msako kwenye nyumba ya Maladyka, maofisa hao walikuta pakiti ya maziwa ya unga. Wenye mamlaka walidai kwamba maziwa hayo ya unga yalifanana na “dawa za kulevya,” basi wakampeleka Ndugu Maladyka na mke wake kwenye hospitali ya watu wenye magonjwa ya akili ili kuwapima. Nataliya aliachiliwa baadaye siku hiyo. Ndugu Maladyka, Ndugu Sakada na Ndugu Zhukov walipelekwa kizuizini. Kisha siku iliyofuata walipelekwa mahabusu

  2. Machi 23, 2021

    Ndugu Sakada aliachiliwa kutoka mahabusu na akawekwa kwenye kifungo cha nyumbani. Alivishwa kifaa kinachoonyesha mahali popote anapoenda, na akakatazwa kutumia Intaneti, kupiga simu, au kuwasiliana na wenzake wanaohusika katika kesi hiyo

  3. Machi 30, 2021

    Ndugu Maladyka aliachiliwa kutoka mahabusu na kuwekwa kwenye kifungo cha nyumbani

  4. Mei 17, 2021

    Ndugu Zhukov aliachiliwa kutoka mahabusu baada ya kuwa huko kwa miezi saba kisha akawekwa kwenye kifungo cha nyumbani

  5. Septemba 30, 2021

    Kesi ya uhalifu ilianza

Maelezo Mafupi Kuwahusu

Tuna uhakika kwamba Yehova ataimarisha mioyo ya ndugu hawa na wengine wote wanaokabili mateso huko Crimea.​—1 Wathesalonike 3:12, 13.