Hamia kwenye habari

Eneo la Ukumbusho la Kambi ya Dachau pamoja na barua ya umma waliomwandikia Rais Putin

JUNI 2, 2021
HABARI ZA ULIMWENGUNI POTE

Kikundi cha Kambi ya Waokokaji wa Dachau Waiomba Urusi Iache Kuwatesa Mashahidi wa Yehova

Kikundi cha Kambi ya Waokokaji wa Dachau Waiomba Urusi Iache Kuwatesa Mashahidi wa Yehova

Kikundi kilichoanzishwa na waokokaji wa kambi ya Dachau, Lagergemeinschaft Dachau kimewaomba wenye mamlaka nchini Urusi waache kuwatesa Mashahidi wa Yehova. Kikundi hicho kimeshutumu kampeni ya nchi hiyo ya kuwatesa ndugu zetu katika barua ya umma waliomwandikia Rais Vladimir Putin tarehe 16 Mei, 2021.

Barua hiyo inasema hivi: “Kila siku kuna ripoti ya jinsi serikali inavyowatesa Mashahidi wa Yehova. Nyumba za watu wa dini hiyo zinafanyiwa msako na kuharibiwa na Idara ya siri ya Urusi, FSB, na polisi. Mashahidi wa Yehova wanakosewa heshima na wanatendewa kwa jeuri. Wanawake na wanaume wanahukumiwa vifungo vya muda mrefu vya gerezani. Kila wanapoomba hali yao iboreshwe wakiwa mahabusu au wakiomba kupewa msamaha, mara nyingi wananyimwa nafasi hiyo.”

Barua hiyo inaishia kwa kusema: “Tunawasihi mmpe kila mkaaji wa Shirikisho la Urusi haki ya kikatiba ya kuabudu kwa uhuru. Tafadhali komesheni ukosefu huu wa haki!”

Kuanzia Mei 2021, kumekuwa na Mashahidi 61 waliofungwa kwa sababu ya imani yao nchini Urusi. Idadi hii inatia ndani watu wenye umri mkubwa kama Dada Valentina Baranovskaya, mwenye umri wa miaka 70, ambaye kwa sasa anatumikia kifungo cha miaka miwili. Alipata kiharusi Julai 2020. Mei 24, 2021, mahakama ilikataa rufaa yake na ya mwana wake Roman Baranovskiy, ambaye anatumikia kifungo cha miaka sita gerezani.

Tunapendezwa na maneno ya watu wanaotazama walio na usawaziko, ambao wameomba hadharani ukosefu huu wa haki dhidi ya ndugu na dada zetu nchini Urusi ukomeshwe. Kwa hakika, tunajua kwamba Yehova atawaokoa watu wake.—Danieli 12:1.