Hamia kwenye habari

SEPTEMBA 16, 2021
HABARI ZA ULIMWENGUNI POTE

Makala za Wakati Unaofaa Kwenye Ukurasa wa Mwanzo wa JW.ORG Zimekuwa na Matokeo

Makala za Wakati Unaofaa Kwenye Ukurasa wa Mwanzo wa JW.ORG Zimekuwa na Matokeo

Ndugu na dada zetu ulimwenguni pote wanatumia makala zilizo kwenye ukurasa wa mwanzo wa jw.org katika huduma na funzo lao la kibinafsi. Hilo limekuwa na matokeo mengi mazuri, kama masimulizi yafuatayo yanavyoonyesha.

Mwangalizi wa mzunguko nchini Kanada anasema kwamba katika miezi michache ya kwanza ya janga la corona, asilimia 75 ya wahubiri katika mzunguko wake waliwaonyesha watu makala yenye kichwa “Nikabilianaje na Upweke?” Kwa mfano, dada mmoja aliwatumia wafanyakazi wenzake kiunganishi cha makala hiyo. Baadhi yao walimshukuru sana kwa makala hiyo.

Dada mwingine nchini Togo ambaye pia mume wake ni mwangalizi wa mzunguko aliwatumia watu wake wa ukoo na marafiki kiunganishi cha makala “Wapanda Farasi Wanne wa Ufunuo.” Sasa anaongoza mafunzo saba ya Biblia kwa sababu ya kufanya hivyo.

Janga la COVID-19 limewalazimisha wanafunzi katika nchi fulani kuhudhuria shule kupitia video iliyounganishwa kwenye mtandao. Dada mmoja mchanga huko Skandinavia alishukuru kwa makala yenye kichwa “Ninawezaje Kusoma kwa Kutumia Mtandao Nikiwa Nyumbani?” Makala hiyo ilitoa mapendekezo yanayofaa kwa wanafunzi wanaojifunza kupitia mtandao. Dada huyo alisema hivi: “Makala hii ilitokea wakati ambapo nilikuwa nimeanza kushindwa kumaliza kazi zangu za shule. Lakini nilipotumia mapendekezo yaliyo katika makala hiyo mambo yalianza kuwa sawa.”

Zaidi ya watumiaji 1,600,000 hutembelea ukurasa wa mwanzo wa jw.org kila siku.

Tunamshukuru Yehova kwa makala hizo ambazo hutusaidia katika funzo letu la kibinafsi na pia ‘kutimiza kikamili huduma yetu.’—2 Timotheo 4:5.