APRILI 21, 2022
HABARI ZA ULIMWENGUNI POTE
Mamilioni Waungana Kuadhimisha Ukumbusho wa Kifo cha Kristo
Aprili 15, 2022, mamilioni ya Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote na wale walioalikwa walikumbuka Mlo wa Jioni wa Bwana. Hiyo ilikuwa mara ya kwanza kuadhimisha Ukumbusho pamoja katika Jumba la Ufalme tangu mwaka wa 2019. Wale ambao hawakufaulu kuhudhuria kwenye Jumba la Ufalme waliunganishwa kwa njia ya mtandao.
Ukumbusho wa kifo cha Kristo ni tukio muhimu sana ambalo Mashahidi wa Yehova hufanya kila mwaka. Kwa sababu ya ugonjwa wa COVID-19, tukio hili la kila mwaka lilifanywa kupitia video mtandaoni kwa miaka miwili mfululizo. Zaidi ya watu milioni 21 walihudhuria Ukumbusho wa mwaka wa 2021.
Kwa baadhi ya watu, kama vile Markensia Remy nchini Haiti, ilikuwa mara yake ya kwanza kuhudhuria Ukumbusho katika Jumba la Ufalme. Markensia ambaye alibatizwa mwaka mmoja uliopita anasema hivi: “Nina furaha sana kwa kuwa nimehudhuria Ukumbusho katika Jumba la Ufalme. Hata siwezi kuelezea furaha yangu. Ninahisi kwamba mimi ni sehemu ya familia ya pekee.”
Tunamshukuru sana Yehova kwa baraka zake katika mwadhimisho wa Ukumbusho wa mwaka huu, na hasa tunamshukuru sana Yehova na Mwana wake, Yesu Kristo, kwa wonyesho mkubwa zaidi wa upendo ambao tumewahi kuonyeshwa.—Yohana 3:16.
Argentina
Bolivia
Brazili
Kambodia
Jamhuri ya Afrika ya Kati
Visiwa vya Cook (Rarotonga)
Ekuado
Indonesia
Israel
Japani
Kazakhstan
Kosovo
Mexico
Paraguai
Peru
Filipino
Poland
Rumania
Hispania
Taiwan
Ukrainia
Marekani
Venezuela