Hamia kwenye habari

Ndugu na dada ambao wamefungwa gerezani nchini Urusi na Crimea

JANUARI 3, 2022
HABARI ZA ULIMWENGUNI POTE

Mataifa Kadhaa Yatoa Tangazo la Pamoja Yakidai Mateso Dhidi ya Mashahidi wa Yehova Yakomeshwe

Mataifa Kadhaa Yatoa Tangazo la Pamoja Yakidai Mateso Dhidi ya Mashahidi wa Yehova Yakomeshwe

Desemba 17, 2021, mataifa kadhaa ambayo ni washirika wa Muungano wa Kimataifa wa Kutetea Uhuru wa Kidini au Imani a (IRFBA) walitoa tangazo la pamoja kuunga mkono Mashahidi wa Yehova wanaoteswa kwa sababu ya imani yao. Tangazo hilo lilisema kwamba Mashahidi wote waliofungwa waachiliwe na pia mateso, unyanyasaji, uvamizi wa nyumba, na ubaguzi dhidi ya Mashahidi ukomeshwe.

Ulimwenguni pote, zaidi ya Mashahidi 150 wa Yehova wamefungwa kwa sababu ya imani yao katika maeneo kama vile Crimea, Eritrea, Singapore, Tajikistan, na Urusi. Mataifa washirika wa IRFBA walisema “wanahangaishwa sana” na “kuongezeka kwa mateso dhidi ya Mashahidi wa Yehova” na wakatangaza kwamba Mashahidi wana haki ya kutenda kupatana na imani yao “bila kuogopa, kunyanyaswa, kubaguliwa, au kuteswa.”

Tunathamini sana serikali zinazofuata haki zinapotetea haki yetu ya ibada. Kwa ujumla, tunajua kwamba Yehova ataendelea kuwalinda ndugu na dada zetu wanaoteswa na ambao wanamtegemea kikamili, naye ‘atawapa amani inayodumu.’​—Isaya 26:3.

a Muungano huo ni mtandao wa nchi zilizoazimia kutetea uhuru wa ibada au imani ulimwenguni pote.