Hamia kwenye habari

Kutoka kushoto hadi kulia: Toleo la kwanza la The Golden Age (1919), toleo la kwanza la Consolation (1937), Toleo la kwanza la Amkeni! (1946), na nakala ya kielektroni ya Amkeni! toleo Na. 2 2019

OKTOBA 1, 2019
HABARI ZA ULIMWENGUNI POTE

Miaka Mia Moja ya Gazeti la Amkeni!

Miaka Mia Moja ya Gazeti la Amkeni!

Gazeti la Amkeni! lilifikisha miaka mia moja mnamo Oktoba 1, 2019. Hili ni mojawapo ya magazeti yanayotafsiriwa na kusambazwa kwa wingi zaidi duniani, nakala zaidi ya milioni 280 huchapishwa kila mwaka katika lugha 211. Amkeni! linashika nafasi ya pili kuchapishwa baada ya gazeti la Mnara wa Mlinzi.

Ndugu Samuel Herd, mshiriki wa Baraza Linaloongoza anasema: “Amkeni limefanya watu wapendezwe na ujumbe wa Biblia kupitia mada mbalimbali zinazozungumziwa. Ijapokuwa muonekano wa gazeti hilo umebadilika kwa miaka mingi, bado linaendelea kuwa kifaa chenye matokeo mazuri katika kazi yetu ya kuhubiri. Kufikisha kwa miaka mia moja ya gazeti hili ni jambo lenye kufurahisha, na ni ushahidi wa msaada wa roho takatifu ya Mungu.”

Kwa mara ya kwanza, Mashahidi wa Yehova walitoa gazeti The Golden Age (jina la awali la gazeti Amkeni!) wakati wa kusanyiko la kihistoria huko Cedar Point, Ohio, Marekani, mnamo Septemba 1919. Mwaka wa 1937, jina la gazeti hilo lilibadilishwa na kuwa Consolation ili kukazia uhitaji wa watu kupata faraja. Hatimaye, mwaka 1946, gazeti lilibadilishwa jina na kuitwa Amkeni! ili kuwasisitizia wasomaji kwamba wanapaswa kuona umuhimu wa kiroho wa siku tunazoishi.

Mnamo Agosti 11, 1946, wahudhuriaji wa kusanyiko la hadharani la Mashahidi wa Yehova lililofanyika Cleveland, Ohio, wakionyesha nakala zao za gazeti jipya la Amkeni! lililotolewa

Tunafurahia kufikia kilele hiki tunapoendelea kutumia gazeti la Amkeni! katika kazi yetu ya elimu ya Biblia ‘tukitoa ushahidi kamili kuhusu habari njema.’—Matendo 20:24.