DESEMBA 8, 2022
HABARI ZA ULIMWENGUNI POTE
Ndugu Dubovenko na Ndugu Litvinyuk Wahukumiwa Miaka Sita Gerezani
Novemba 30, 2022, Mahakama ya Jiji la Armyanskiy iliyo katika Jamhuri ya Crimea iliwahukumu Ndugu Aleksandr Dubovenko na Ndugu Aleksandr Litvinyuk. Ndugu wote wawili walihukumiwa kifungo cha miaka sita gerezani na kupelekwa gerezani moja kwa moja.
Maelezo Mafupi Kuwahusu
Tunafarijiwa kujua kwamba sikuzote Yehova yuko kando yetu, popote tulipo na wakati wowote tunapokabili majaribu.—Zaburi 139:7-12.
Mfuatano wa Matukio
Agosti 2, 2021
Kesi ya uhalifu ilifunguliwa. Ndugu wote wawili walishtakiwa kwa kutumia programu za kufanya mikutano kupitia video mtandaoni kuendeleza utendaji wa shirika lenye msimamo mkali
Agosti 5, 2021
Misako ilifanywa katika nyumba za familia nane za Mashahidi wa Yehova kutia ndani nyumba ya familia ya Dubovenko na ya Litvinyuk. Ndugu Litvinyuk alikamatwa na kupelekwa mahabusu
Agosti 6, 2021
Ndugu Litvinyuk aliachiliwa kutoka mahabusu na kuwekwa chini ya kifungo cha nyumbani
Agosti 9, 2021
Maofisa wa polisi walifanya tena msako katika nyumba ya Dubovenko. Aleksandr alihojiwa na kuwekwa chini ya kifungo cha nyumbani
Agosti 11, 2021
Ndugu Litvinyuk alishtakiwa rasmi kwamba alipanga utendaji wa shirika lenye msimamo mkali
Februari 8, 2022
Ndugu Dubovenko alishtakiwa rasmi kwamba alipanga utendaji wa shirika lenye msimamo mkali
Aprili 29, 2022
Kesi ya uhalifu ilianza. Hakimu alikataa ombi la Ndugu Litvinyuk la kumwona daktari na kupata matibabu alipokuwa chini ya kifungo cha nyumbani
Septemba 8, 2022
Ndugu wote wawili waliruhusiwa kuondoka nyumbani kila siku kati ya saa moja asubuhi na saa moja jioni
Novemba 30, 2022
Ndugu wote wawili walihukumiwa kifungo cha miaka sita gerezani