Hamia kwenye habari

MACHI 19, 2014
HABARI ZA ULIMWENGUNI POTE

Guy H. Pierce, Mshiriki wa Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova, Amekufa Akiwa na Umri wa Miaka 79

Guy H. Pierce, Mshiriki wa Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova, Amekufa Akiwa na Umri wa Miaka 79

Guy H. Pierce, mshiriki wa Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova katika makao yao makuu ya ulimwenguni pote huko Brooklyn, New York, alikufa Jumanne, Machi 18. Alikuwa na umri wa miaka 79.

Mbali na mke wake, Penny, Bw. Pierce ameacha watoto sita, wajukuu kadhaa pamoja na vitukuu. Atakumbukwa sana na Mashahidi wa Yehova kote duniani ambao aliwaona kama familia.

Katika taarifa, washiriki wenzake wa Baraza Linaloongoza walisema hivi: “Maisha yake ya uhodari na uaminifu alipokuwa duniani yataendelea kutuimarisha kadiri miaka inavyopita.”

Wanahabari Wanaweza Kuwasiliana na:

J. R. Brown, Ofisi ya Habari za Umma, simu +1 718 560 5000

 

Soma Zaidi