Hamia kwenye habari

MACHI 20, 2014
HABARI ZA ULIMWENGUNI POTE

Mashahidi wa Yehova Wataanza Kampeni ya Ulimwenguni Pote ya Kuwaalika Watu Kwenye Ukumbusho wa Kifo cha Kristo

Mashahidi wa Yehova Wataanza Kampeni ya Ulimwenguni Pote ya Kuwaalika Watu Kwenye Ukumbusho wa Kifo cha Kristo

NEW YORK—Jumamosi, Machi 22, 2014, Mashahidi wa Yehova wataanza kampeni ya ulimwenguni pote ya kuwakaribisha watu kwenye tukio muhimu zaidi la mwaka: Ukumbusho wa kifo cha Kristo. Mwaka uliopita, watu 19,241,252 walihudhuria tukio hilo la pekee. Mashahidi wa Yehova wanatumaini kwamba mwaka huu watu wengi zaidi watahudhuria Ukumbusho huo ambao utafanyika Jumatatu, Aprili 14, baada ya jua kutua.

J. R. Brown, msemaji wa Mashahidi wa Yehova kwenye makao yao makuu ya ulimwenguni pote yaliyoko New York anasema: “Tuna hakika kwamba wote watakaohudhuria Ukumbusho pamoja nasi watafurahia sana tukio hilo na kufaidika kutokana nalo. Hilo linatuchochea kuwakaribisha watu wengi kadiri tuwezavyo ili waje kuhudhuria tukio hili takatifu.”

Wanahabari Wanaweza Kuwasiliana na:

J. R. Brown, Ofisi ya Habari za Umma, simu +1 718 560 5000