Hamia kwenye habari

(Kushoto) Hatua zinazofaa za kujilinda zinatia ndani kusafisha kwa ukawaida maeneo yanayoguswa mara nyingi nyumbani na kwenye Jumba la Ufalme; (Katikati) Katika maeneo fulani yaliyoathiriwa, wahubiri wanaweza kuamua kushiriki katika aina nyingine za huduma, kama vile kuhubiri kupitia simu; (Kulia) Katika maeneo yaliyoathiriwa, ikitegemea hali za kwenu, wazee wanaweza kufanya mipango ili wahubiri watazame mikutano iliyorekodiwa

MACHI 3, 2020
HABARI ZA ULIMWENGUNI POTE

Habari za Karibuni Kuhusu Virusi vya Corona na Jinsi ya Kujilinda

Habari za Karibuni Kuhusu Virusi vya Corona na Jinsi ya Kujilinda

Makao Makuu ya ulimwenguni pote ya Mashahidi wa Yehova, yanafuatilia kwa ukaribu mlipuko wa ugonjwa wa virusi vya Corona (unaojulikana kama COVID-19). Kutokana na unabii wa Biblia, tunajua kwamba magonjwa ya kuambukiza ni mojawapo ya mambo yanayooonyesha kwamba tunaishi katika siku za mwisho. (Luka 21:11) Kunapokuwa na mlipuko wa ugonjwa ni jambo la hekima kuchukua hatua za kujilinda na kuwalinda wengine.—Methali 22:3.

Huenda wengine wakajiuliza, akina ndugu na dada katika maeneo yaliyoathiriwa wanaendeleaje. Mlipuko wa ugonjwa wa korona umelazimu ofisi za tawi nchini na makutaniko nchini Italia Japani, Korea Kusini na nchi nyingine, kufanya mabadiliko fulani. Katika visa fulani ofisi ya tawi imefuta mipango ya kuwatembeza wageni. Katika visa vingine serikali imezuia watu wasikusanyike katika vikundi vikubwa na hilo limefanya ofisi ya tawi ifute makusanyiko ya mzunguko. Mbali na hilo, makutaniko yamelazimika kufanya mabadiliko kuhusiana na huduma na mikutano ya kutaniko katika baadhi ya maeneo. Licha ya changamoto, hizo ndugu zetu wanaendelea kujijenga kiroho na kutiana moyo.—Yuda 20, 21.

Katika hali hizo ndugu zetu wamenufaika kwa kufuata kanuni zifuatazo. Mambo hayo yanaweza kukusaidia wewe na familia yako ikiwa mtakabili mlipuko wa ugonjwa huo katika eneo lenu.

  • Usiwe na Hofu. Ingawa ni muhimu kuwa chonjo ugonjwa unapotokea na kuchukua tahadhari, tunapaswa kutenda kwa kutegemea habari zilizothibitishwa, si woga.—Methali 14:15; Isaya 30:15.

  • Fuata mapendekezo na miongozo ya serikali. Mara nyingi wenye mamlaka hutoa tahadhari na kuweka vizuizi ili kulinda afya za watu. Ni muhimu kupata habari kutoka serikalini na kufuata miongozo inayotolewa.—Waroma 13:1.

  • Dumisha Usafi. Ni muhimu kunawa mikono yako kwa ukawaida kwa kutumia sabuni na maji au dawa ya kunawa mikono. Pia, nyumbani na kwenye Jumba la Ufalme tunapaswa kusafisha kwa ukawaida maeneo yanayoguswa mara nyingi. Isitoshe, wataalamu wa afya wanapendekeza kwamba si vizuri kusalimiana kwa mikono katika hali hizo kwa sababu kufanya hivyo kunaweza kueneza ugonjwa huo. Kuhusu ugonjwa wa corona, shirika la afya ulimwenguni limetoa mwongozo wa ziada.

  • Waonyeshe wengine Upendo. Ingawa tunajua umuhimu wa kuhudhuria mikutano ya Kikristo na kushiriki katika kazi za kuhubiri, ikiwa una ugonjwa huo vizuri kukaa nyumbani ili usiwaambukize wengine. Hilo linaonyesha upendo na linawalinda ndugu na dada zetu na majirani wetu ambao si Mashahidi.—Mathayo 22:39.

  • Fuata Mabadiliko ya Muda Kuhusu Mipango ya Kutaniko. Katika maeneo yaliyo na mlipuko wa ugonjwa huenda ofisi ya tawi ikalazimika kufuta kwa muda mikutano ya kutaniko, makusanyiko, na matukio mengine ya kitheokrasi. Imekuwa hivyo katika maeneo yaliyoathiriwa sana ugonjwa wa corona kama vile maeneo fulani nchini Italia, Japani, na Korea Kusini. Ikitegemea hali za eneo lenu, wazee wanaweza kufanya mipango ili wahubiri watazame mikutano iliyorekodiwa wakiwa nyumbani. Wahubiri wanaweza kuhubiri kwa kupiga simu, kuandika ujumbe wa simu, barua pepe, au kuandika barua.