Hamia kwenye habari

APRILI 30, 2015
HABARI ZA ULIMWENGUNI POTE

Mashahidi wa Yehova Watangaza Makusanyiko ya 2015 Yatakayoanza Mei

Mashahidi wa Yehova Watangaza Makusanyiko ya 2015 Yatakayoanza Mei

NEW YORK—Mashahidi wa Yehova waanza mfululizo wa makusanyiko ya 2015 nchini Marekani kuanzia Mei 22. Kusanyiko la Eneo la “Mwigeni Yesu!” la 2015 litafanywa ulimwenguni pote hadi mwezi wa Januari 2016. Katika kila eneo la kusanyiko, Mashahidi watafanya kampeni ya majuma matatu ya kuwaalika watu katika programu hiyo bila malipo.

J. R. Brown, msemaji wa Mashahidi wa Yehova kutoka kwenye makao makuu Brooklyn, New York, alisema hivi: “Kichwa cha kusanyiko la mwaka huu kinakazia umaarufu wa Yesu ulimwenguni pote na kielelezo chake bora kwa watu wenye umri, malezi na tamaduni mbalimbali. Tunatarajia kwamba watu watafurahia njia hii mpya ya ufafanuzi wa matukio muhimu katika maisha ya Yesu. Programu ya mwaka huu itatia ndani video zenye kufundisha na kusisimua zitakazoonyesha jinsi tunavyoweza kufaidika kwa kumwiga Yesu katika maisha yetu ya kila siku.”

Tarehe hususa na mahali ambapo Makusanyiko ya Eneo ya “Mwigeni Yesu!” ya 2015 yatafanywa zinapatikana katika tovuti rasmi ya Mashahidi wa Yehova, jw.org/sw. Waandishi wa habari wanaweza kuwasiliana na ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova iliyo karibu nao kwa habari zaidi, kutia ndani jina la anayewasiliana na waandishi wa habari.

Wanahabari Wanaweza Kuwasiliana na:

J. R. Brown, Ofisi ya Habari za Umma, simu +1 718 560 5000