Hamia kwenye habari

AGOSTI 1, 2014
HABARI ZA ULIMWENGUNI POTE

Mashahidi Wafanya Kampeni ya Kutangaza Tovuti Iliyotafsiriwa Katika Lugha Nyingi Zaidi Ulimwenguni, JW.ORG

Mashahidi Wafanya Kampeni ya Kutangaza Tovuti Iliyotafsiriwa Katika Lugha Nyingi Zaidi Ulimwenguni, JW.ORG

NEW YORK—Agosti 1, 2014, Mashahidi wa Yehova wataanza kampeni ya mwezi mzima ya kusambaza ulimwenguni pote trakti mpya yenye kichwa Tutapata Wapi Majibu ya Maswali Muhimu Maishani? ili kuwafahamisha watu kuhusu Tovuti yao rasmi, jw.org. Inapatikana katika lugha 500 hivi, ina machapisho yanayoweza kupakuliwa katika lugha 700 hivi, na jw.org ndiyo Tovuti iliyotafsiriwa katika lugha nyingi zaidi duniani.

Zaidi ya watu milioni moja hutembelea Tovuti ya jw.org kila siku. Tovuti hiyo ina makala na video zenye mashauri yanayowafaa watu wa kila umri, malezi, na hali. Mojawapo ya video hizo, yenye kichwa Kwa Nini Ujifunze Biblia? itaunganishwa na alama ya QR iliyo kwenye trakti hiyo mpya. Video hiyo inatumia picha za matukio halisi pamoja na vibonzo ili kuonyesha manufaa halisi ya kujifunza Biblia. Kwa sasa, video hiyo inapatikana katika lugha zaidi ya 450, na tangu ilipotolewa Novemba 18, 2013, imepakuliwa mara milioni 4 hivi.

J. R. Brown, msemaji wa Mashahidi wa Yehova katika makao yao makuu ya Brooklyn, New York, anasema hivi: “Tumesisimuka sana kwa sababu ya kampeni hii. Kuna Mashahidi wa Yehova milioni nane hivi ulimwenguni pote, na sote tutaongea na jirani zetu kuhusu Tovuti hii. Huenda hii ndiyo itakayokuwa kampeni kubwa zaidi ambayo tumewahi kupanga.”

Geoffrey Jackson, mshiriki wa Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova, anasema hivi: “Tangu Tovuti hii ilipoanzishwa miaka miwili iliyopita, watu ulimwenguni pote wamethamini sana maktaba hii. Kwenye Tovuti hii, unaweza kutazama video zinazoweza kuwasaidia watoto wako, utapata makala zinazoweza kusaidia familia yako, na hata kusoma Biblia kwenye mtandao. Tunataka watu wengi kadiri iwezekanavyo wanufaike kutokana na jw.org, na ndio sababu tulipanga kampeni hii ya pekee.”

Wanahabari Wanaweza Kuwasiliana na:

J. R. Brown, Ofisi ya Habari za Umma, simu +1 718 560 5000