Hamia kwenye habari

MACHI 6, 2018
HABARI ZA ULIMWENGUNI POTE

Mashahidi Waanza Kampeni ya Kila Mwaka ya Kuwaalika Watu Kwenye Ukumbusho wa Kifo cha Kristo

Mashahidi Waanza Kampeni ya Kila Mwaka ya Kuwaalika Watu Kwenye Ukumbusho wa Kifo cha Kristo

Machi 3, 2018, Mashahidi wa Yehova walianza kampeni ya ulimwenguni pote ya kusambaza mialiko ya Mlo wa Jioni wa Bwana, unaojulikana pia kuwa Ukumbusho wa kifo cha Kristo. Mashahidi katika nchi 240 watakusanyika kwa ajili ya tukio hilo la Machi 31, ambalo wanaliona kuwa muhimu zaidi katika mwaka. Watu wanaalikwa pia kuhudhuria hotuba ya pekee ya Biblia yenye kichwa “Yesu Kristo Ni Nani Hasa?” itakayotolewa juma la Machi 19.

David A. Semonian, msemaji wa Mashahidi wa Yehova, anasema hivi: “Mwaka wa 2017, watu zaidi ya milioni 20 walihudhuria Ukumbusho, milioni 12 kati yao hawakuwa Mashahidi. Kwa hiyo, Ukumbusho ni tukio muhimu, si kwa Mashahidi wa Yehova tu, bali kwa mamilioni ya wageni ulimwenguni pote. Lengo letu ni kwamba majirani wetu wote wapate mwaliko wa kuhudhuria tukio hilo mahali patakapowafaa.”

Wanahabari Wanaweza Kuwasiliana na:

David A. Semonian, Ofisi ya Habari za Umma, +1-845-524-3000