Hamia kwenye habari

MACHI 20, 2015
HABARI ZA ULIMWENGUNI POTE

Watu Milioni Ishirini Watazamiwa Kuhudhuria Ukumbusho

Watu Milioni Ishirini Watazamiwa Kuhudhuria Ukumbusho

NEW YORK—Baada ya jua kutua Ijumaa, Aprili 3, 2015, Mashahidi wa Yehova wataadhimisha Ukumbusho wa Kifo cha Kristo, tukio muhimu zaidi kwao katika mwaka. Mwadhimisho huo unatia ndani hotuba ya watu wote ya dakika 45 yenye kichwa “Onyesha Shukrani kwa Mambo Ambayo Kristo Amekufanyia!” Majuma machache kabla ya tukio hilo muhimu, Mashahidi watashiriki katika kampeni ya ulimwenguni pote ya kuwaalika majirani, marafiki, na watu wa familia wahudhurie tukio hilo.

J. R. Brown, msemaji wa Mashahidi wa Yehova katika makao yao makuu Brooklyn, New York, anasema hivi: “Mwaka jana, Mashahidi wa Yehova milioni 8 hivi waliwaalika watu kwenye Ukumbusho wa Kifo cha Kristo, na jumla ya karibu watu milioni 20 walihudhuria. Mwaka huu tunatarajia idadi kubwa zaidi.”

Wanahabari Wanaweza Kuwasiliana na:

J. R. Brown, Ofisi ya Habari za Umma, simu +1 718 560 5000