Hamia kwenye habari

MEI 1, 2018
HABARI ZA ULIMWENGUNI POTE

Makusanyiko ya Kila Mwaka ya Mashahidi wa Yehova ya 2018 Yataanza Mwezi wa Mei

Makusanyiko ya Kila Mwaka ya Mashahidi wa Yehova ya 2018 Yataanza Mwezi wa Mei

NEW YORK—Ijumaa, Mei 18, 2018, Mashahidi wa Yehova wataanza mfululizo wa makusanyiko yao ya kila mwaka. Kichwa cha kusanyiko la mwaka huu ni “Uwe Jasiri!” Kabla ya tukio hilo kuanza, Mashahidi ulimwenguni pote watashiriki katika kampeni ya ulimwenguni pote ya kuwakaribisha watu wote kuhudhuria programu hiyo bila malipo. Makusanyiko yatafanywa kwenye maeneo 180 katika nchi mbalimbali.

Programu hiyo ya siku tatu itakuwa na sehemu 54 zitakazotia ndani hotuba, drama za kusikiliza, mahojiano, na video fupifupi. Isitoshe, sinema kuu yenye kichwa Simulizi la Yona—Somo Kuhusu Ujasiri na Rehema itaonyeshwa siku ya mwisho ya kusanyiko hilo. Kila siku, vipindi vya asubuhi na alasiri vitaanza kwa video za muziki zilizotayarishwa hasa kwa ajili ya kusanyiko hilo.

David A. Semonian, msemaji wa Mashahidi wa Yehova, anasema hivi: “Unapotazama habari leo, unaweza kuona wazi kwamba watu wa umri wote wanakabili mahangaiko na mambo yenye kuogopesha zaidi kuliko wakati mwingine. Unahitaji ujasiri ili kukabiliana na mikazo hiyo. Tunawakaribisha wote kwenye kusanyiko la mwaka huu ili wanufaike kutokana na mashauri yanayofaa yanayopatikana katika Biblia.”

Habari kuhusu tarehe na mahali ambapo kila kusanyiko litafanyiwa zinapatikana kwenye tovuti rasmi ya Mashahidi, jw.org/sw.

Wanahabari Wanaweza Kuwasiliana na:

David A. Semonian, Ofisi ya Habari za Umma, +1-845-524-3000