Hamia kwenye habari

JUNI 4, 2014
HABARI ZA ULIMWENGUNI POTE

Mashahidi Waanza Makusanyiko ya Kimataifa

Mashahidi Waanza Makusanyiko ya Kimataifa

NEW YORK—Kusanyiko la kwanza katika mfululizo wa makusanyiko ya kimataifa ya siku tatu ya Mashahidi wa Yehova yenye kichwa “Endeleeni Kuutafuta Kwanza Ufalme wa Mungu!” yataanza asubuhi ya Ijumaa, Juni 6, 2014, katika uwanja wa Ford Field huko Detroit, Michigan, Marekani. Sehemu fulani za programu hiyo zitasikilizwa moja kwa moja katika maeneo mengine huko Arizona, California, Florida, Illinois, Missouri, New Jersey, na North Carolina, na zitatafsiriwa katika Kialbania, Kikorea, Kipolandi, na Kireno.

J. R. Brown, msemaji wa Mashahidi wa Yehova katika makao yao makuu ya ulimwenguni pote huko Brooklyn, New York, anasema hivi: “Kwa muda wa majuma matatu yaliyopita, Mashahidi jijini Detroit na majiji yatakayounganishwa kusikiliza programu kwa njia ya video wamekuwa wakiwaalika majirani wao kuhudhuria tukio hilo muhimu sana. Jijini Detroit, tunatarajia umati mkubwa wa wahudhuriaji wapatao 45,000, kutia ndani wajumbe zaidi ya 2,000 kutoka Australia, Kanada, Taiwan, na Ujerumani.”

Katika kipindi chote cha kiangazi nchini Marekani, Mashahidi watakuwa na makusanyiko 16 ya kimataifa kwenye viwanja vikubwa katika majimbo kumi mbalimbali. Katika maeneo fulani, programu hiyo itafanywa yote au kwa sehemu katika Kiajemi, Kialbania, Kiarabu, Kiarmenia, Kichuukese, Kifaransa, Kigiriki, Kihindi, Kihispania, Kiiloko, Kiindonesia, Kiitaliano, Kijapani, Kikantoni, Kikorea, Kikrioli cha Haiti, Kimandarini, Kipolandi, Kirumania, Kirusi, Kisamoa, Kitagalogi, Kitwi, Kivietnam, Lugha ya Ishara ya Marekani, na Lugha ya Visiwa vya Marshall. Kuanzia Juni 2014 na kuendelea hadi mwaka wa 2015, Mashahidi watakuwa na makusanyiko ya kimataifa nchini Australia, Ekuado, Korea Kusini, Mexico, Uingereza, Ujerumani, Ugiriki, na Zimbabwe.

Wanahabari Wanaweza Kuwasiliana na:

J. R. Brown, Ofisi ya Habari za Umma, simu +1 718 560 5000