Urusi
Wataalamu Waeleza: Urusi Yatumia kwa Hila Sheria ya Kudhibiti Vikundi Vyenye Msimamo Mkali ili Kuwafanya Mashahidi wa Yehova Waonekane Kuwa Wahalifu
Hii ni sehemu ya 1 ya mfuatano wa mahojiano ya pekee yaliyo na sehemu tatu pamoja na wasomi maarufu wa mambo ya dini, siasa, na soshiolojia na pia wataalamu wa masomo yanayohusu Urusi ilipokuwa sehemu ya Muungano wa Sovieti na ilipojitenga na Muungano wa Sovieti.
Onyo Lilitolewa Dhidi ya Makao Makuu ya Mashahidi Nchini Urusi Latishia Uhuru wa Ibada
Mashahidi wa Yehova nchini Urusi wanaweza kujikuta katika hali itakayowaruhusu wawe huru kuamini chochote wanachotaka lakini wasiruhusiwe kushiriki ibada pamoja na waabudu wenzao.
Wenye Mamlaka Nchini Urusi Wapanga Kufunga Makao Makuu ya Mashahidi wa Yehova
Barua rasmi ya onyo iliyotolewa na wenye mamlaka nchini Urusi ni ishara ya uwezekano wa kupiga marufuku ibada inayofanywa kwa amani na Mashahidi nchini Urusi.
Kamati ya Haki za Kibinadamu ya Umoja wa Mataifa Yaripoti Kwamba Urusi Imeweka Sheria Inayowalenga Hasa Mashahidi wa Yehova ya Kupinga Shughuli Zenye Msimamo Mkali
Kamati ya Haki za Kibinadamu ya Umoja wa Mataifa imesema kwamba mahakama za Urusi zimetumia sheria ya kupinga watu wenye msimamo mkali kuwabagua Mashahidi wa Yehova.
Wenye Mamlaka Nchini Urusi Wapandikiza Ushahidi wa Uwongo Kuwashtaki Mashahidi
Mashahidi wa Yehova katika majiji ya Sevastopol na Balakovo wamefichua mpango wa wenye mamlaka wa kupandikiza machapisho yaliyopigwa marufuku kwenye sehemu zao za ibada na baadaye kuyatumia ili kuwashtaki kuwa wenye msimamo mkali.
Maofisa Nchini Urusi Wakamata Mzigo wa Biblia na Machapisho ya Biblia
Wenye mamlaka wamezuia Biblia na machapisho ya Mashahidi wa Yehova yasiingizwe nchini humo. Kitendo hicho kimewaathirije Mashahidi wa Yehova na raia wengine wa Urusi?
Mahakama ya Taganrog Yawaadhibu Mashahidi kwa Utendaji wa Kidini
Washtakiwa 16 walihukumiwa kwa kuendesha shughuli zenye msimamo mkali. Uamuzi huo umeweka msingi hatari kwa wenye mamlaka kushtaki shughuli za kidini za Mashahidi wa Yehova nchini Urusi licha ya kwamba hazivurugi amani.
Mahakama ya Jiji la Taganrog Yawahukumu Mashahidi wa Yehova kwa Utendaji wa Kidini
Uamuzi huo utasababisha unyanyasaji na mashtaka ya kosa la jinai kwa Mashahidi yaongezeke kotekote nchini Urusi.
Maelezo kuhusu Kesi ya Uhalifu ya Mashahidi wa Yehova Taganrog, Urusi
Tangu 2011, Mashahidi wa Yehova 16 wameshtakiwa isivyo haki kuwa ni wahalifu kwa sababu ya imani yao. Je, ushahidi unaunga mkono mashtaka ya kuwa watu wenye msimamo mkali?