Hamia kwenye habari

Jengo la Mahakama Kuu ya Urusi

NOVEMBA 25, 2021
URUSI

Azimio la Baraza Kuu la Mahakama Kuu ya Urusi—Litamaanisha Nini kwa Mashahidi wa Yehova?

Azimio la Baraza Kuu la Mahakama Kuu ya Urusi—Litamaanisha Nini kwa Mashahidi wa Yehova?

Oktoba 28, 2021, Baraza Kuu la Mahakama Kuu ya Urusi lilifanya marekebisho kuhusu suala la utendaji wenye msimamo mkali. Maneno mapya yaliyotumiwa yanaonyesha kwamba mtu au kikundi cha watu wanaoshiriki ibada hawapaswi kuonwa kuwa wanajihusisha katika utendaji wa shirika lililopigwa marufuku. Hata hivyo, azimio hilo la Baraza Kuu halijazuia mateso dhidi ya Mashahidi wa Yehova, kwa kuwa wenye mamlaka nchini Urusi tayari wametafsiri marekebisho hayo katika njia nyingi tofauti.

Kwa mfano, tangu marekebisho hayo yafanywe Oktoba 28, wenye mamlaka wamevamia nyumba 13 hivi za Mashahidi wa Yehova, wakakataa ombi la rufaa la Dada Irina Lokhvitskaya, na wakamhukumu Dada Yelena Savelyeva aliye na umri wa miaka 80. Tofauti na hilo, Novemba 22, 2021, mahakama huko Vladivostok ilisema kwamba Ndugu Dmitriy Barmakin hana hatia yoyote na ikamwondolea mashtaka yote.

Hatujui ikiwa azimio lililorekebishwa litapunguza mateso au litatokeza vifungo vikali hata zaidi. Vyovyote vile, tunaendelea kumtegemea Yehova kikamili awasaidie ndugu na dada zetu wavumilie kwa shangwe hadi atakapoandaa wokovu wa kweli na wa kudumu.​—Zaburi 146:3-5.