Hamia kwenye habari

Dada Lyudmila Shut

APRILI 30, 2021
URUSI

Dada Mlemavu Mwenye Umri wa Miaka 73 Amtegemea Yehova Anapokabili Kifungo

Dada Mlemavu Mwenye Umri wa Miaka 73 Amtegemea Yehova Anapokabili Kifungo

HABARI YA KARIBUNI | Mahakama ya Urusi Yakataa Ombi la Rufaa

Agosti 25, 2021, Mahakama ya Eneo la Primorye ilikataa ombi la rufaa la Dada Lyudmila Shut. Hukumu yake ya awali itaendelea kutumika. Hatahitaji kwenda gerezani wakati huu.

Mei 19, 2021, Mahakama ya Wilaya ya Nadezhdinskiy katika Eneo la Primorye ilimhukumu Dada Lyudmila Shut mwenye umri wa miaka 73 kifungo cha nje cha miaka minne.

Maelezo Mafupi Kumhusu

Lyudmila Shut

  • Alizaliwa: 1947 (Makarov, Kisiwa cha Sakhalin)

  • Maisha Yake: Alianza kujifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova mapema katika miaka ya 2000. Alipendezwa sana na unabii wa Biblia. Alibatizwa katika mwaka wa 2003. Mume wake alikufa mwaka huohuo. Ana watoto watatu na wajukuu watatu. Matatizo makubwa ya kiafya yanamzuia kutembea bila msaada

Historia ya Kesi

Wenye mamlaka walianza kuwachunguza Mashahidi wa Yehova katika kijiji cha Razdolnoye mnamo Novemba 2017. Februari 2020, wenye mamlaka walifungua kesi ya uhalifu dhidi ya Dada Lyudmila Shut. Licha ya afya yake na matatizo ya afya yanayoonekana waziwazi, walimwekea vizuizi vya kusafiri.

Shughuli za kesi yake zimefanya afya ya kimwili na ya kihisia ya Lyudmila izorote. Uwezo wake wa kuona umepungua hivi kwamba anahitaji kufanyiwa upasuaji na sasa anakabili matatizo ya kukosa usingizi. Lyudmila anasadiki kwamba Yehova anamlinda kwa sababu anamtegemea na kumwamini kabisa. Kama Yehova anavyoahidi kwenye Isaya 26:3, amempa “amani inayodumu.”

Ndugu na dada Wakristo wanamtunza Lyudmila kwa upendo. Anathamini hasa kujua kwamba akina ndugu wanasali kwa ajili yake. Anasema hivi: “Sitawahi kusahau hilo.”

Ingawa mwana wake na binti yake mdogo si Mashahidi wa Yehova, wamemuunga mkono wakati wa kipindi hiki kigumu.

Anaposubiri uamuzi wake, tunasali tukiwa na uhakika kamili kwamba Dada Shut ataendelea “kutegemea nguvu za Mungu.”—2 Timotheo 1:8.