Hamia kwenye habari

Dada Valentina Suvorova akiwa na mume wake, Vladimir

MACHI 9, 2021
URUSI

Dada Mwenye Umri wa Miaka 73 Anaweza Kufungwa kwa Sababu ya Imani Yake

Dada Mwenye Umri wa Miaka 73 Anaweza Kufungwa kwa Sababu ya Imani Yake

Hukumu Inatarajiwa

Mahakama ya Wilaya ya Metallurgichesky iliyoko Chelyabinsk itatangaza hivi karibuni uamuzi wake katika kesi kumhusu Dada Valentina Suvorova. a Mwendesha-mashtaka bado hajatoa maombi ya hukumu.

Maelezo Mafupi Kumhusu

Valentina Suvorova

  • Alizaliwa: 1948 (Sorovskoye, Eneo la Kurgan)

  • Maisha Yake: Alistaafu baada ya kufundisha Shule ya Muziki ya Chelyabinsk kwa miaka 30. Anapenda kutunza bustani, kucheza dansi, na kusikiliza muziki

    Alifunga ndoa na Vladimir mnamo 1973. Mwana wao, Igor, alikufa miaka michache iliyopita kutokana na kansa. Hivi karibuni mama yake na dada yake walikufa pia

Historia ya Kesi

Machi 26, 2019, maofisa wa polisi waliokuwa na bunduki walivamia zaidi ya nyumba 20 za ndugu zetu katika maeneo ya Chelyabinsk na Yemanzhelinsk. Desemba 5, 2019, baada ya uchunguzi mrefu, Valentina, ambaye sasa ana umri wa miaka 73, alihukumiwa kuwa mhalifu kwa sababu ya kusoma Biblia na kuwahubiria wengine. Kwa sasa amewekewa vizuizi vya kusafiri. Pia Vladimir ameshtakiwa kuwa mhalifu kwa sababu ya imani yake ya Kikristo.

Valentina anakumbuka kilichotokea maofisa wenye bunduki walipovamia nyumba yao walipokuwa wakilala: “Hatukuruhusiwa kuoga, kuchana nywele, au kuvaa nguo zinazofaa. Walirusha vitu huku na kule na kuangalia katika kila sehemu, kila kabati, sanduku, kipochi, na mfuko. . . . Waliangalia ndani ya sufuria, hata waliangalia kwenye pazia na matandiko. Hakuna sehemu waliyokosa kuchunguza.”

Valentina anahofu kwamba mateso hayo yatamwathiri sana kwa sababu ya umri wake na afya yake.

Valentina anasema kwamba ratiba yake ya kujifunza Biblia kwa ukawaida ilimsaidia kuwa imara. Anasema: “Kuchunguza andiko la siku, kutafakari mambo niliyosoma, na kuyatumia kulinisaidia kuvumilia majaribu hayo.”

Valentina anaongezea kwamba kutayarisha na kuhudhuria mikutano, funzo la kibinafsi, na ibada ya familia zilitimiza fungu muhimu ili kuvumilia hali hizo zenye mkazo. Anasema: “Ninajifunza jambo jipya kwenye kila mkutano kisha ninajaribu kulitumia.” Anasema kwamba sala zenye unyoofu humfariji sana, kisha anaongezea, “Sikuzote ninamshukuru Mungu kwa msaada wake.”

Isitoshe, Valentina anaendelea kujikumbusha na kuwakumbusha wengine hivi: “Hakuna sababu ya kuogopa chochote. Uwe imara na mwenye nguvu katika imani, na ukumbuke Mathayo 6:33 na 2 Wakorintho 1:3, 4.”

Ni wazi kwamba ndugu na dada zetu nchini Urusi, kutia ndani Valentina na Vladimir, wanathibitisha ukweli wa Zaburi 64:10: “Mwadilifu atashangilia kwa sababu ya Yehova na kumkimbilia; wote walio wanyoofu moyoni watashangilia.”

a Tarehe ya hukumu haitolewi mapema nyakati zote.