Hamia kwenye habari

Dada Nataliya Kriger pamoja na mume wake, Valeriy

FEBRUARI 25, 2021
URUSI

Dada Nataliya Kriger Anakabili Kifungo Kutokana na Uvamizi wa “Siku ya Hukumu”

Dada Nataliya Kriger Anakabili Kifungo Kutokana na Uvamizi wa “Siku ya Hukumu”

HABARI ZA KARIBUNI | Mahakama ya Urusi Yakataa Rufaa

Novemba 25, 2021, Mahakama katika Eneo Lililotengewa Wayahudi ilikataa rufaa ya Dada Nataliya Kriger. Hukumu yake ya awali itaendelea kutumika. Hahitaji kwenda gerezani wakati huu.

Julai 30, 2021,Mahakama ya Wilaya ya Birobidzhan iliyo katika Eneo Lililotengewa Wayahudi ilimhukumu Dada Kriger. Mahakama ilimhukumu kifungo cha nje cha miaka miwili na miezi sita.

Maelezo Mafupi Kumhusu

Nataliya Kriger

  • Alizaliwa: 1978 (Khabarovsk)

  • Maisha Yake: Mama yake alikufa Nataliya alipokuwa mtoto mchanga. Alilelewa katika makao ya watoto yatima. Alipokuwa na umri wa miaka sita, alihamia kilomita 400 kwenda Amurzet, Urusi. Aliishi huko pamoja na nyanya, shangazi, na binamu yake. Wote ni Mashahidi wa Yehova. Alifanya kazi ya kutunza wenye umri mkubwa

  • Mwaka wa 1999 alibatizwa na kuwa Shahidi wa Yehova. Aliolewa na Valeriy mwaka wa 2017. Wanapenda kucheza dansi, kuendesha mashua ndogo kwenye mto, na kupanda milima

Historia ya Kesi

Mei 2018, wenye mamlaka nchini Urusi walifanya msako katika nyumba ya familia ya Kriger. Msako huo ulikuwa sehemu ya kampeni ambayo wenye mamlaka waliita “Siku ya Hukumu.” Mwendesha-mashtaka alifungua kesi ya uhalifu dhidi ya Valeriy baada ya msako huo. Februari 6, 2020, mamlaka zilifungua kesi ya uhalifu dhidi ya Nataliya. Alikuwa miongoni mwa dada sita walioshtakiwa siku hiyo.

Mbali na mashtaka ya uhalifu anayokabili, Nataliya anahuzunika kwa sababu ya kumpoteza nyanya yake katika kifo, aliyekufa Februari 2020. Alikuwa amemtunza nyanya yake kwa miaka sita.

Uhusiano wenye nguvu na Yehova unamsaidia Nataliya kuvumilia majaribu hayo. Anasema hivi: “Kusali kwa ajili ya wengine hunisaidia kuepuka kukazia fikira matatizo yangu. Yehova amenikaribia zaidi na amekuwa halisi kwangu kupitia jaribu hili. Ninajionea wazi akijibu sala zangu na akinitegemeza.”

Mara nyingi Nataliya hutafakari sababu nyingi zinazompa uhakika kwamba Yehova ataendelea kumtegemeza. Anasema hivi: “Zaburi 94:14 huniimarisha sana inaposema: ‘Ulinifariji na kunibembeleza.’ Kuna mifano mingi ya kale na ya wakati wetu inayoonyesha watumishi wa Mungu jasiri waliovumilia majaribu. Kutafakari mifano hiyo huniimarisha sana.”