Hamia kwenye habari

Dada Yelena Reyno-Chernyshova

JANUARI 28, 2021
URUSI

Dada Yelena Reyno-Chernyshova Anakabili Kifungo kwa Sababu ya Imani Yake

Dada Yelena Reyno-Chernyshova Anakabili Kifungo kwa Sababu ya Imani Yake

Hukumu Inatarajiwa

Januari 29, 2021, a Mahakama ya Wilaya ya Birobidzhan katika Eneo Lililotengewa Wayahudi, inatarajiwa kutangaza uamuzi wake katika kesi inayomhusu Dada Yelena Reyno-Chernyshova. Mwendesha-mashtaka bado hajatuma maombi ya hukumu.

Maelezo Mafupi Kumhusu

Yelena Reyno-Chernyshova

  • Alizaliwa: 1968 (Maloy, Eneo la Irkutsk)

  • Maisha Yake: Alijifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova katika miaka ya 1990. Mambo aliyojifunza yalimchochea aache utumishi wa kijeshi na ajitahidi kuboresha ndoa yake. Alibatizwa mwaka wa 1998

  • Ijapokuwa mume wake si Shahidi wa Yehova, anaunga mkono uamuzi wake wa kumtumikia Yehova. Dada Yelena anapenda kucheza mpira wa miguu na mpira wa wavu

Historia ya Kesi

Septemba 29, 2019, wenye mamlaka katika eneo la Birobidzhan walifungua kesi ya uhalifu dhidi ya Dada Yelena Reyno-Chernyshova.

Maofisa wenye kutisha wa Idara ya Usalama wa Taifa (FSB), walifanya msako katika nyumba ya Yelena. Anamshukuru Yehova kwa kumsaidia kuwa mtulivu. Anakumbuka hivi: “Nilisali kwa Yehova bila kuacha anipatie utulivu na ujasiri, ili niweze kujiendesha vizuri, na niendelee kuwa mwaminifu. Msako ulifanywa katika hali ya utulivu, na kila mtu alikuwa mpole.”

Kesi hiyo imemwathiri sana Yelena na familia yake. Mume wake alipatwa na mshtuko wa moyo (kwa mara ya tatu) Julai 2020. Wenye mamlaka wamempiga marufuku Yelena kusafiri nje ya Birobidzhan. Wamezuia pia akaunti zake za benki.

Yelena ameendelea kuwa imara kwa kutafakari jinsi watumishi wengine wa Yehova walivyoshughulika na mateso. Anasema hivi: “Ninapenda kusoma ripoti kuhusu ndugu na dada ambao nyumba zao zilivamiwa na wale ambao waliteswa kwa sababu ya kumwamini Yehova. Ingawa walikabili changamoto nyingi na mateso, kwa ujasiri walivumilia hali hizo zote.” Amenufaika pia kwa kusoma na kutafakari Biblia kila siku.

Huku akiendelea kuvumilia hali yake, Yelena anapenda kutafakari andiko la Isaya 30:15. Linasema hivi kwa sehemu: “Mtakuwa na nguvu mkiendelea kuwa watulivu na kuwa na tumaini.” Anasema hivi: “Mimi hutafakari mara nyingi mstari huo. Ninamshukuru sana Yehova kwa kunivuta kwake! . .  Sikuzote nina amani ya moyo. Ninamwamini [Yehova] hata zaidi na kumtegemea kabisa katika mambo yote. Nina uhakika kwamba hataniacha kamwe.”

a Huenda Itabadilika.