Hamia kwenye habari

Ndugu Denis Merkulov akiwa na mke wake, Nataliya

DESEMBA 27, 2022 | HABARI ZILIONGEZWA: MACHI 27, 2023
URUSI

HABARI ZA KARIBUNI—APIGWA FAINI | “Tunapokabili Majaribu, Yehova Mwenyewe Anatupa Nguvu”

HABARI ZA KARIBUNI—APIGWA FAINI | “Tunapokabili Majaribu, Yehova Mwenyewe Anatupa Nguvu”

Machi 23, 2023, Mahakama ya Jiji la Apatity iliyo katika Eneo la Murmansk ilimhukumu Ndugu Denis Merkulov. Alitozwa faini ya rubo 500,000 (dola 6,485.00 za Marekani).

Maelezo Mafupi Kumhusu

Tunafajirika kujua kwamba hata tukikabili majaribu ya aina gani, maadamu tuna uhusiano mzuri na Yehova na tunamtegemea, ‘atatufanya tuwe imara na atatutia nguvu.’​—1 Petro 5:10.

Mfuatano wa Matukio

  1. Julai 21, 2021

    Maofisa walifanya msako katika nyumba 14 za Mashahidi wa Yehova katika jiji la Apatity. Maofisa wa FSB walivamia nyumba ya Merkulov na kuwapeleka wenzi hao kituoni ili kuwahoji. Waliwaruhusu kurudi nyumbani kesho yake saa 10 alfajiri

  2. Julai 22, 2021

    Maofisa wa upelelezi walimwita Denis tena. Aliwekwa kizuizini

  3. Julai 23, 2021

    Aliachiliwa na kuwekwa kwenye kifungo cha nyumbani

  4. Septemba 17, 2021

    Aliondolewa kifungo cha nyumbani na kuwekewa vizuizi vya kusafiri

  5. Julai 15, 2022

    Alishtakiwa kwa kupanga utendaji wa shirika lenye msimamo mkali hasa “kuimba nyimbo” na “kusali kwa Yehova Mungu”

  6. Septemba 20, 2022

    Kesi ya uhalifu ilianza