Hamia kwenye habari

Mahakama ya Wilaya ya Kuznetskiy ya Novokuznetsk iliyo katika Eneo la Kemerovo

FEBRUARI 20, 2023 | HABARI ZIMEONGEZWA: JULAI 14, 2023
URUSI

HABARI ZA KARIBUNI—DADA AHUKUMIWA | “Hakuna Jambo Linaloweza Kunishinda”

HABARI ZA KARIBUNI—DADA AHUKUMIWA | “Hakuna Jambo Linaloweza Kunishinda”

Julai 11, 2023 Mahakama ya Wilaya ya Kuznetskiy iliyo Novokuznetsk ilimhukumu Dada Lyubov Serebryakova kifungo cha nje cha miaka minne. Hahitaji kwenda gerezani wakati huu.

Maelezo Mafupi Kumhusu

Lyubov anamtegemea Yehova akiwa na uhakika kwamba ‘atatenda kwa niaba yake.’ Ametuwekea mfano mzuri ambao tunaweza kuiga tunapokabili majaribu kama hayo.​—Zaburi 37:5.

Mfuatano wa Matukio

  1. Novemba 2019-2020

    Maofisa wa polisi walikuwa wakiwafuatilia kisiri baadhi ya Mashahidi wa Yehova walio Novokuznetsk kwa kutumia vifaa vya kurekodi sauti na video

  2. Julai 8, 2022

    Uchunguzi ulianza kufanywa maofisa walipogundua kwamba Lyubov alikuwa akihudhuria mikutano ya Mashahidi wa Yehova na pia kuzungumza na wengine kuhusu Biblia

  3. Julai 26, 2022

    Alishtakiwa kwa kushiriki katika utendaji wa shirika lenye msimamo mkali. Aliwekewa vizuizi vya kusafiri

  4. Septemba 21, 2022

    Kesi ya uhalifu ilianza

a Hatukupata picha ya Dada Serebryakova makala hii ilipokuwa ikitayarishwa.