Hamia kwenye habari

Dada Irina Mikhaylenko

DESEMBA 9, 2022 | HABARI ZILIONGEZWA: APRILI 25, 2023
URUSI

HABARI ZA KARIBUNI—DADA APIGWA FAINI | “Ninapata Amani kwa Kusali kwa Bidii Kutoka Moyoni”

HABARI ZA KARIBUNI—DADA APIGWA FAINI | “Ninapata Amani kwa Kusali kwa Bidii Kutoka Moyoni”

Aprili 25, 2023, Mahakama ya Wilaya ya Metallurgicheskiy iliyo Chelyabinsk ilimhukumu Dada Irina Mikhaylenko. Alipigwa faini ya rubo 120,000 (dola 1,471 za Marekani).

Maelezo Mafupi Kumhusu

Tunatiwa moyo na bidii anayoonyesha Irina na jinsi anavyomtegemea Yehova. Yehova anaendelea kuulinda “uhai wa washikamanifu wake.”​—Zaburi 97:10.

Mfuatano wa Matukio

  1. Machi 26, 2019

    Msako ulifanywa kwenye nyumba kumi za Mashahidi wa Yehova wanaoishi katika eneo la Chelyabinsk, kutia ndani nyumba ya Irina

  2. Agosti 31, 2021

    Kesi ya uhalifu ilifunguliwa

  3. Oktoba 22, 2021

    Nyumba yake ilifanyiwa msako tena. Alichukuliwa ili kuhojiwa. Wenye-mamlaka wakamwekea vizuizi vya kusafiri

  4. Oktoba 27, 2021

    Alishtakiwa rasmi kwa kushiriki katika utendaji wa shiriki lililopigwa marufuku

  5. Septemba 7, 2022

    Kesi ya uhalifu ilianza