JULAI 14, 2021 | HABARI ZILIONGEZWA: DESEMBA 2, 2022
URUSI
HABARI ZA KARIBUNI—HUKUMU YATANGAZWA | Kujitayarisha kwa Ajili ya Mateso Kunawasaidia Ndugu Watatu Kudumisha Ushikamanifu
Novemba 30, 2022, Mahakama ya Wilaya ya Ussuriyskiy katika Eneo la Primorye imewahukumu Ndugu Anton Chermnykh, Ndugu Sergey Korolchuk, na Ndugu Dmitriy Tishchenko vifungo vya nje vya miaka sita. Hawahitaji kwenda gerezani wakati huu.
Mfuatano wa Matukio
Septemba 23, 2020
Kesi dhidi ya Anton, Sergey, na Dmitriy ilianza kusikilizwa mahakamani
Julai 7, 2020
Anton, Sergey, na Dmitriy walishtakiwa rasmi kwa kuwa viongozi wa shirika la kidini lililopigwa marufuku na lenye “msimamo mkali”
Juni 18, 2019
Sergey aliwekwa mahabusu kwa siku mbili
Maelezo Mafupi Kuwahusu
Kesi yao inapoendelea kusikilizwa, tunajua kwamba Yehova atabariki uaminifu wa Anton, Sergey, na Dmitriy.—Methali 28:20.