Hamia kwenye habari

Kushoto hadi kulia: Dada Irina Sidorova, Dada Matrena Spiriadi, na Ndugu Aleksandr Verguno

DESEMBA 28, 2021
URUSI

HABARI ZA KARIBUNI |Mashahidi Waaminifu Wanajionea Utegemezo wa Yehova

HABARI ZA KARIBUNI |Mashahidi Waaminifu Wanajionea Utegemezo wa Yehova

Aprili 4, 2022, Mahakama ya Jiji la Abakan katika Jamhuri ya Khakassia iliwahukumu Dada Matrena Spiriadi na Ndugu Aleksandr Vergunov. Kila mmoja wao amehukumiwa kifungo cha nje cha miaka miwili na nusu. Kwa kusikitisha, Dada Irina Sidorova, ambaye hapo awali alikuwa ameshtakiwa katika kesi hii, alikufa. Matrena na Aleksandr hawahitaji kwenda gerezani wakati huu.

Mfuatano wa Matukio

  1. Machi 30, 2021

    Maofisa wa usalama walifanya upekuzi katika nyumba ya Matrena na Aleksandr

  2. Julai 17, 2020

    Irina alikufa kutokana na matatizo yaliyotokea baada ya upasuaji

  3. Mei 20, 2020

    Wenye mamlaka walimhoji Irina, kwa sababu ya kushuku alihusika katika kile walichosema ni utendaji wenye msimamo mkali

  4. Mei 19, 2020

    Wenye mamlaka walimhoji Aleksandr, kwa sababu ya kushuku alihusika katika kile walichosema ni utendaji wenye msimamo mkali

  5. Aprili 20, 2020

    Kesi ya uhalifu ilifunguliwa dhidi ya Aleksandr, Irina, na Matrena

Maelezo Mafupi Kuwahusu

Tuna uhakika kwamba Mungu wetu, Yehova anawaona na kuwathamini watumishi wake wote washikamanifu. Tunajua kwamba hatakosa kuwatunza watumishi hao anaowapenda sana.​—Isaya 49:15.