DESEMBA 28, 2021
URUSI
HABARI ZA KARIBUNI |Mashahidi Waaminifu Wanajionea Utegemezo wa Yehova
Aprili 4, 2022, Mahakama ya Jiji la Abakan katika Jamhuri ya Khakassia iliwahukumu Dada Matrena Spiriadi na Ndugu Aleksandr Vergunov. Kila mmoja wao amehukumiwa kifungo cha nje cha miaka miwili na nusu. Kwa kusikitisha, Dada Irina Sidorova, ambaye hapo awali alikuwa ameshtakiwa katika kesi hii, alikufa. Matrena na Aleksandr hawahitaji kwenda gerezani wakati huu.
Mfuatano wa Matukio
Machi 30, 2021
Maofisa wa usalama walifanya upekuzi katika nyumba ya Matrena na Aleksandr
Julai 17, 2020
Irina alikufa kutokana na matatizo yaliyotokea baada ya upasuaji
Mei 20, 2020
Wenye mamlaka walimhoji Irina, kwa sababu ya kushuku alihusika katika kile walichosema ni utendaji wenye msimamo mkali
Mei 19, 2020
Wenye mamlaka walimhoji Aleksandr, kwa sababu ya kushuku alihusika katika kile walichosema ni utendaji wenye msimamo mkali
Aprili 20, 2020
Kesi ya uhalifu ilifunguliwa dhidi ya Aleksandr, Irina, na Matrena
Maelezo Mafupi Kuwahusu
Tuna uhakika kwamba Mungu wetu, Yehova anawaona na kuwathamini watumishi wake wote washikamanifu. Tunajua kwamba hatakosa kuwatunza watumishi hao anaowapenda sana.—Isaya 49:15.